HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 14, 2019

KAMPUNI YA JERVOIS YAONESHA NIA KUWEKEZA KABANGA

Waziri wa Madini Doto Biteko amekutana na Wawakilishi wa Kampuni ya Jervois Mining Limited ya Australia ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika mradi wa Nikel- Colbat, Kabanga.  Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Biteko ameendelea kusisitiza kuhusu kufuatwa kwa Sheria na taratibu kwa wenye nia ya kuwekeza katika Sekta ya Madini na kueleza kuwa, kwa upande wa Wizara, inafanya jitihada za kuondoa urasimu kwenye uwekezaji katika sekta husika.

“ Tunataka mwekezaji mwenye nia anapoonesha dhamira ya kuwekeza baada ya taratibu zote kukamilika basi aanze mara moja,” amesema Waziri Biteko. Akizungumza katika kikao hicho mmoja wa wawakilishi wa kampuni hiyo Balozi Mstaafu Andrew Mcalister, amesema kuwa, nchi ya Tanzania inaweza kuwa mzalishaji mkubwa wa madini ya Colbat kutokana na ubora wake na mazingira ya uwekezaji yaliyopo nchini ikiwemo uwazi.
Mbali na Waziri Biteko, wengine waliohudhuria kikao hicho ni Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, na wataalam wengine wa wizara.
 Waziri wa Madini Doto Biteko (kulia) akimsikiliza mwakilishi wa kampuni ya Jervois Mining Limited ya Australia   Balozi Mstaafu Andrew Mcalister (katikati). Kushoto ni Naibu Waziri Stanslaus Nyongo. Wengine ni wawakilishi wa kampuni hiyo.
 Waziri wa Madini Doto Biteko akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jervois Mining Limited ya Australia Brye Croker.
Baadhi ya Wataalam wa Wizara ya Madini wakifuatilia kikao baina ya Waziri wa Madini na wawakilishi wa kampuni ya Jervois Mining Limited.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad