HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, January 6, 2019

POLEPOLE ACHARUKA UZINDUZI WA KAMPENI KATA YA MAGOMENI ASEMA WAPINZANI WANABWABWAJA TU

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Humphrey Polepole amefungua Kampeni na kumnadi mgombea Udiwani wa kata ya Magomeni, Shaweji Mkubura, katika Viwanja vya Magomeni Makuti.

Akifungua Kampeni hizo Polepole amewaambia wakazi wa magomeni kuchagua mgombea kutoka CCM kwani Wapinzani wameishiwa sera wanabwabwaja tu mitandaoni na kuisema vibaya Tanzania kwa mataifa Rafiki.

“siku zote Mnyororo huwa unafanana sasa ni aibu kama mtachagua wapinzani ambao wao kazi yao kubwabwaja kila kukicha kuanzia mitandaoni kazi kuisema vibaya serikali yetu aitoshi wamesafiri kwenda nje kutusema vibaya kana kwamba awaoni Maendeleo yanayoletwa na Mwenyekiti wa chama chetu”alisema Polepole

“Mzee mwenye Madevu ametembea nchi za ulaya wa marafiki zetu kuwasihii wasitusadie baada ya ziara hiyo tukasikia nchi kadhaa zinatuchimba mkwara kwa mambo yanayotuhusu wenyewe matokeo yake wakatuambia kama unataka msaada lazima tufuate sera za ushoga jambo ambalo serikali ya CCM Imegomea”.

Alisema Sasa chama cha uliberali ambacho hakieleweki kina Makatibu wawili,Wenyeviti wawili na mlengo wao kila kitu hewala, hivyo wao suala la vijana wa kiume kuvaa madela kwao ni sawa tu hivyo sio watu wakuwachagua.

Polepole alisema kuwa CCM inayoongozwa na Rais Magufuli inamleta kwenu Shaweji kwa wakazi wa kata ya Magomeni waweze kumchagua ifikapo January 19 aweze kuwaongoza wakazi wa magomeni.Alimaliza kwa kusema kuwa Magomeni ndipo waktoka watoto wa Mjini hivyo wakazi wa magonei awatakiwi kukosea kwa kupiga kura kwa wapinzani bali wanatakiwa kupeleka kura zote kwa shaweji.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Humphrey Polepole, akimnadi Mgombea Udiwani wa CCM Kata ya Magomeni Ndugu Shaweji Mkumbura wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo Jijini Dar es Salaam leo.
Mgombea Udiwani wa Kata ya Magomeni kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Ndugu Shaweji Mkumbura akiwa amepiga magoti kuomba kura kwa wakazi wa Magomei waliofika katika uzinduzi wa kampeni zake zilizofanyika katika Viwanja vya Magomeni Makuti Jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Humphrey Polepole, akihutubia wakazi wa Kata ya Magomeni eneo la Magomeni Makuti wakati akimuombea kura Mgombea wa CCM aweze kuchaguliwa kuwa Diwani katika wa kata hiyo.
Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Kate Kamba akizungumza na wakazi wa kata ya Magomeni eneo la Makuti B kumnadi Mgombea udiwani wa kata hiyo kupitia CCM
MNEC wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam , Yusuph Nassoro akihutubia wakazi wa Magomeni wakati wa uzinduzi wa Kampeni za udiwani wa kata hiyo
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Mkoa wa Dar es SalaaSimon Mwakifamba akipokea kadi na kumkaribisha Mwanachama Mapya wa CCM kutoka Chadema
Baadhi ya Wanachama waliofika katika Mkutano huio wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa udiwani kata ya Magomeni

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad