Meneja ukuzaji Masoko wa TBL na ABInBev Afrika Mashariki Edith Bebwa (katikati) akimkabidhi ufunguo wa gari mkazi wa Arusha, George Issaya mshindi wa gari la promosheni iliyomalizika ya TBL Kumenoga Tukutane Baa.
Mkazi wa Arusha, George Isaya (29) ambaye wiki iliyopita aliibuka mshindi wa gari mpya aina ya Renault KWID, katika droo ya promosheni ya ‘TBL Kumenoga, Tukutane Baa’leo amekabidhiwa gari katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Akiongea wakati wa hafla hiyo, Meneja wa Huduma za Masoko wa TBL, David Tarimo, alisema gari hilo ndio la mwisho katika promosheni hii iliyodumu kwa kipindi cha miezi mitatu ambayo pia imewezesha wateja wengine Julitha Kilawe wa Dar es Salaam na Frank Nathan wa Iringa kujishindia magari.
No comments:
Post a Comment