HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 3, 2018

ESRF yafanya darasa la wazi kuhusiana na mfumo wa kidigitali kuelekea tanzania ya viwanda

Mtaalamu wa Masuala ya Kidigitali, Profesa Louis Henry Fourie, akiwasilisha mada iliyohusu mchango wa kidigitali katika Maendeleo ya Viwanda akihusisha fursa zinazopatikana katika Kilimo, Elimu, Biashara na Uwasilishaji wa Huduma wakati wa darasa la wazi lililofanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Faustin Kamuzora akichangia hoja wakati Darasa la Wazi lililohusu Mchango wa Kidigitali katika Maendeleo ya Viwanda likihusisha  fursa zinazopatikana katika Kilimo, Elimu, Biashara na Uwasilishaji wa Huduma. Darasa hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Maarifa na Ubunifu, Margareth Nzuki akichangia hoja wakati Darasa la Wazi lililohusu Mchango wa Kidigitali katika Maendeleo ya Viwanda likihusisha  fursa zinazopatikana katika Kilimo, Elimu, Biashara na Uwasilishaji wa Huduma. Darasa hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mtaalamu wa Masuala ya Kidigitali, Profesa Louis Henry Fourie na katikati ni Dkt. Oswald Mashindano.
Mshiriki akichangia hoja wakati Darasa la Wazi lililohusu Mchango wa Kidigitali katika Maendeleo ya Viwanda likihusisha  fursa zinazopatikana katika Kilimo, Elimu, Biashara na Uwasilishaji wa Huduma. Darasa hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa Masuala ya Kidigitali, Profesa Louis Henry Fourie(wapili kushoto),akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Darasa la Wazi lililohusu  Mchango wa Kidigitali katika Maendeleo ya Viwanda likihusisha  fursa zinazopatikana katika Kilimo, Elimu, Biashara na Uwasilishaji wa Huduma.Wengine mstari wa mbele ni Dkt. Oswald Mashindano(wakwanza kushoto) Mkuu wa Kitengo cha Maarifa na Ubunifu, Margareth Nzuki (watatu kushoto) na Profesa Mascalena . Darasa hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad