HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 29, 2018

Wafanyakazi bora wa mwezi Oktoba JKCI wapongezwa

 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happiness Kusekwa akipokea zawadi ya Daktari bora wa mwezi Oktoba kutoka kwa Mkurugenzi wa Tiba ya Moyo na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya utoaji zawadi kwa wafanyakazi bora iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo. Zawadi hizo zilitolewa na kampuni ya dawa za binadamu ya Samiro
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimkabidhi zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi Oktoba Afisa Muuguzi Msaidizi Keyness Erasmus Mng’anya wa JKCI wakati wa hafla fupi ya utoaji zawadi kwa wafanyakazi bora iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo. Zawadi hizo zilitolewa na kampuni ya dawa za binadamu ya Samiro. Picha na: Genofeva Matemu - JKCI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad