HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 30, 2018

Serikali ya Misri yawasilisha andiko la kwanza la nia ya kuwekeza nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Misri hapa nchini Bibi. Nevine El-Saeed pamoja na kupokea andiko la awali la nia ya serikali ya Misri kutaka kuwekeza nchini katika sekta ya mifugo.

Kaimu Balozi wa Misri ambaye ameambatana na Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim katika ofisi ndogo za wizara ya mifugo na uvuvi zilizopo jijini Dar es Salaam, amesema serikali ya nchi hiyo inahitaji kuwekeza ili kufungua fursa mbalimbali ambazo zitapatikana kupitia uwekezaji huo.

Akizungumza na maafisa hao pamoja na wajumbe waliohudhuria kikao hicho, Katibu Mkuu Ole Gabriel amesema nchi ya Tanzania ina mifugo mingi na kwamba ikitumika vizuri kupitia uwekezaji, ambapo nia ya serikali ya awamu ya tano imejikita zaidi kupitia kufufua na kuanzishwa kwa viwanda vipya kutaongeza fursa nyingi zaidi zikiwemo za ajira.

Aidha, amesema nia yake ni kuhakikisha anasimamia nia ya serikali ya Misri kufanikisha uwekezaji huo ambao anasema wizara yake itahakikisha inaweka mazingira yatakayofanya uwekezaji huo uwe endelevu na kuleta tija kwa nchi zote mbili.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na wakuu wa idara zilizo chini ya ofisi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wawakilishi kutoka Dawati la Sekta Binafsi, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Kituo cha Kuendeleza kilimo Nyanda za juu Kusini (SAGCOT) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa maelezo kwa Kaimu Balozi wa Misri nchini Bibi. Nevine El-Saeed na Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim katika ofisi ndogo za wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel  Kaimu Balozi wa Misri nchini Bibi. Nevine El-Saeed na Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim, wakati akiongoza kikao cha namna bora ya uwekezaji wa serikali ya Misri katika sekta ya mifugo nchini (wajumbe wa mkutano huo hawapo pichani).
 Wajumbe wa kikao kuhusu nia ya serikali ya Misri kuwekeza katika sekta ya mifugo nchini wakifuatilia mazungumzo ya kikao hicho. Wajumbe hao wanatoka idara zilizo chini ya Wizara ya Mifyugo na Uvuvi, Dawati la Sekta Binafsi, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Kituo cha Kuendeleza Kilimo Nyanda za Juu Kusini (SAGCOT) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel akipokea andiko la awali la nia ya serikali ya Misri kuwekeza nchini katika sekta ya mifugo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi wa Misri hapa nchini Bw. Mohamed Ibrahim.
  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel, Kaimu Balozi wa Misri nchini Bibi. Nevine El-Saeed na Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim mara baada ya kuahirishwa kwa kikao kinachohusu nia ya serikali ya Misri kuwekeza katika sekta ya mifugo nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi wa Misri nchini Bibi. Nevine El-Saeed, Mkuu wa Idara ya Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim na wajumbe waliohudhuria kikao kujadili nia ya serikali ya Misri kuwekeza katika sekta ya mifugo. Kikao kimefanyika katika ofisi ndogo za wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad