Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akiwa ameambatana na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa wakati alipotembelea ofisi za DAWASA Bunju Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa akipewa taarifa na mfanyakazi wa DAWASA kitengo cha kuunganisha wateja wapya, Chini akieleza jambo kwa muhudumu huyo kuhusiana na utaratibi wa kuunganisha wateja wapya.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji akizungumza na kuwasikiliza wananchi waliokwenda kupata huduma kwenye ofisi za DAWASA Bunju Jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment