HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 30, 2018

Gulio la TCRA kuelimisha umma juu ya matumizi bora ya huduma za mawasiliano lafana

Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imesema kuwa wananchi wanatakiwa kutumia Mawasiliano kwa maendeleo. Hayo ameyasema Mkuu wa Kitengo cha Watumiaji wa Mawasiliano wa TCRA Thadayo Ringo wakati wa Gulio lililofanyika kata Ilembo mkoani Mbeya amesema kuwa mawasiliano yameleta fursa kwa wananchi hivyo watumie katika kujiletea maendeleo.

Amesema kuwa katika uchumi wa viwanda hivyo watumie katika kutangaza biashara au bidhaa wanazozalisha viwandani. "TCRA itaendelea kutoa elimu katika kuhakikisha kila mwananchi anatumia mawasiliano katika kujiletea uchumi na sio kutumia kwa matumizi yasiyo na faida"amesema
Aidha amesema kuwa katika Gulio katika sehemu mbalimbali wameambata na watoa huduma za mawasiliano, pamoja na Jeshi la Polisi ili kutoa elimu kwa wananchi hao.

 Wananchi wa Kata ya Ilembo wakiwa kwenye banda la TCRA baada ya kuwasogezea huduma za za utoaji huduma ya mawasiliano  wakati wa Gulio la TCRA la kuelimisha umma juu ya matumizi bora ya huduma za mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad