HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 27, 2018

BENKI YA CRDB YAMTAMBULISHA MKURUGENZI MTENDAJI WAKE NCHINI BURUNDI

 Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay aliyemtembelea Ikulu ya Bujubura, kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (kulia). Rais Nkurunziza alipongeza uteuzi wa Mkurugenzi huyo na kumtakia mafanikio zaidi katika kazi yake na kumuomba kuongeza matawi ya Benki hiyo nchini Burundi ili watu wawe na utamaduni wa kuhifadhi fedha zao benki na sio kuzihifadhi ndani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza jambo wakati alipomtembelea Naibu Katibu Mkuu wa Chama tawala cha CNDD-FDD nchini Burundi, Balozi Joseph Ntakirutimana (kulia) ikiwa ni semu ya ziara yake ya kujitambulisha tangu ateuliwe kushika nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay 
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama tawala cha CNDD-FDD nchini Burundi, Balozi Joseph Ntakirutimana akifafanua jambo wakati akizungumza na Ujumbe wa Benki ya CRDB uliomtembelea ofisini kwake, jijini Bujumbura, Burundi hivi karibuni.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama tawala cha CNDD-FDD nchini Burundi, Balozi Joseph Ntakirutimana (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela katika viwanja vya makao makuu ya chama hicho, jijini Bujumbura, Burundi. Kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Burundi, Bruce Mwile.
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dkt. Edmund Kitokezi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyemtembelea Ubalozini, jijini Bujumbura nchini Burundi.
Gavana wa Benki Kuu ya Burundi, Jean Ciza (kushoto) akiwa katika mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay aliyemtembelea ofisini kwake Bujubura, kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (kulia).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) akifurahi jambo na Gavana wa Benki Kuu ya Burundi, Jean Ciza (kulia) pamoja na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Burundi, Melchior Wagara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akieleza jambo kwa Mmoja wa Wateja wakubwa wa Benki ya CRDB nchini Burundi na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Interpetrol, Tariq Bashir.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad