HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 9, 2018

WAZIRI MKUU AWAONYA WALIMU KUTOJIHUSISHA NA WIZI WA MITIHANI

*Asisitiza kwamba vitendo hivyo vinawadharirisha
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaonya maafisa elimu na walimu kutojihusisha na vitendo vya wizi wa mitihani vinavyofanywa kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi kwa sababu vinawadharirisha.

“Kama kweli umemuandaa mtoto huna sababu ya kuiba mitihani na mtoto hawezi kufikiria kuiba mitihani kwa sababu yuko nje ya mfumo. Walimu heshimuni maadili ya kazi ya ualimu.”

Waziri Mkuu ametoa onyo hilo leo (Jumanne, Oktoba 9, 2018) baada ya kukabidhiwa vyumba vya madarasa vya shule za msingi Nyakato na Kashozi, wilayani Bukoba.

Vyumba hivyo vilivyojengwa kwa msaada wa Serikali ya Japan baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera mwaka 2016.

Waziri Mkuu amesema tathmini ya elimu katika shule za msingi na sekondari hufanyika kwa kufanya mitihani, dosari ya udanganyifu wa mitihani iliyojitokeza katika mitihani ya darasa la saba mwaka huu isijirudie tena.

Wiki iliyopitaBaraza la Mitihani la Taifa (NECTA) lilifuta matokeo ya mitihani ya darasa la saba kwa shule za msingi zote za Halmashauri ya Chemba na baadhi ya shule katika halmashauri ya Kondoa, Kinondoni, Mwanza jiji na Ubungo kwa kosa la kuvujisha mitihani.

Waziri Mkuu amesema tayari Serikali imechukua hatua kali kwa watu wote walioshiriki katika kitendo hicho kwa sababu kinadumaza uelewa na ufikiri kwa wanafunzi, hivyo kuwaandaa watoto kuwa wategemezi.

“Hata hivyo, Serikali inaendelea na uchunguzi juu ya suala hili ili kubaini chanzo cha wizi huo. Walimu, kitendo cha kumpa mtoto mitihani ni sawa na kujiaibisha kwani mnaonekana hamjafanya kazi zenu ipasavyo. Sitarajii kusikia suala hili tena.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametembelea kiwanda cha kahawa cha Amimza ambacho ni kati ya viwanda vikubwa vitano vya kusindika kahawa Barani Afrika, ambapo ametumia fursa hiyo kumpongeza mwekezaji mzawa Bw. Amiri Hamza na kumuhamasisha aongeze uzalishaji.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametembelea  kituo cha utafiti Maruku ambapo alikagua na kupokea taarifa za shughuli za utafiti wa zao la kahawa na alitumia fursa hiyo kuwashauri wakulima wenye miti mikongwe kung’oa na kupanda mipya kwa awamu.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikata utepe ikiwa ni ishara ya kupokea madarasa mapya yaliyojengwa kwa Masada wa serikali ya Japan katika Shule ya Msingi ya Nyakato wilayani Bukoba, Oktoba 8, 2018. Kulia kwake ni Mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini,    Katsutoshi Takeda. Majengo ya shule hiyo yaliharibiwa na tetemeko la ardhi lililoukumba mkoa wa Kagera.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikata utepe ikiwa ni ishara ya kufungua madaras mapya yaliyojengwa kwa Masada wa serikali ya Japan katika Shule ya Msingi ya Nyakato wilayani Bukoba, Oktoba 8, 2018. Kushoto ni Mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini,    Katsutoshi Takeda (kushoto). Majengo ya shule hiyo yaliharibiwa na tetemeko la ardhi lililoukumba mkoa wa Kagera.(
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini, Bw. Katsutoshi Takeda wakiwa kwenye moja ya madarasa yaliyojengwa kwa ufadhili wa serikali ya Japan katika shule ya msingi ya Nyakato wilayani Bukoba ambayo iliharibiwa na tetemeko la ardhi. Madarasa hayo yalikabidhiwa kwa Waziri Mkuu, Oktoba 9, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi baada ya kupokea madarasa yaliyojengwa kwa masada wa serikali ya Japan katika shule ya msingi ya Nyakato wilayani Bukoba ambayo iliharibiwa na tetemeko la ardhi la Kagera. Madarasa hayo yalikabidhiwa kwa Waziri Mkuu na Mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini, Bw. Katsutoshi Takeda, Oktoba 9, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea funguo kutoka kwa Mwakilishi wa Balozi wa Japan Nchini, Katsutoshi Takeda  ikiwa ni ishara ya kukabidhiwa madarasa yaliyojengwa na serikali ya Japan katika Shule ya Msingi ya Nyakato wilayani Bukoba, Oktoba 9, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wanafunzi baada ya kupokea madarasa yaliyojengwa kwa masada wa serikali ya Japan katika shule ya msingi ya Nyakato wilayani Bukoba ambayo iliharibiwa na tetemeko la ardhi la Kagera. Madarasa hayo yalikabidhiwa kwa Waziri Mkuu na Mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini, Bw. Katsutoshi Takeda, Oktoba 9, 2018.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad