HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 3, 2018

WAZIRI MHAGAMA AKUTANA NA WATENDAJI WA OFISI YAKE KUJADILI UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2015-2020

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo kwa Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vilivyopo chini ya Ofisi hiyo (hawapo pichani) alipokutana nao kujadili utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 na Maagizo ya Mhe. Rais Dkt.John Magufuli aliyoyatoa katika kikao cha kufungua Bunge la kumi na moja la tarehe 20 Novemba 2015 kilichofanyika Ukumbi wa LAPF Jijini Dodoma Oktoba 1, 2018 Kulia kwake ni Naibu wake anayeshughulikia wenye Ulemavu Mhe.Stella Ikupa na kushoto kwake Mhe.Anthony Mavunde anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vilivyopo chini ya Ofisi hiyo wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Maagizo ya Mhe. Rais aliyoyatoa katika kikao cha kufungua Bunge, Jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akielezea jambo kwa Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Ofisi yake (hawapo pichani) wakati wa Kikao kazi hicho.
 Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Peter Kalonga, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, akiwasilisha hoja kwa Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa kujadili utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 na Maagizo ya Mhe. Rais Dkt.John Magufuli aliyoyatoa katika kikao cha kufungua Bunge la Kumi na Moja Novemba 2015.
 Baadhi ya Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vilivyopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu wakisililiza maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokutana nao kujadili utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi na Maagizo ya Mhe. Rais aliyoyatoa katika kikao cha kufungua Bunge la tarehe 20 Novemba,  2015.
Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi akielezea jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Maagizo ya Mhe. Rais aliyoyatoa katika kikao cha kufungua Bunge la kumi na moja la tarehe 20 Novemba, 2015 walipokutana Oktoba 1, 2018 Dodoma.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad