HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 9, 2018

Wachimbaji Wadogowadogo Watakiwa Kuzingatia Taratibu Upatikanaji wa Leseni

 Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko akisalimiana na viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Simanjiro mara baada ya kuwasili wilayani hapo kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja kutembelea eneo la wachimbaji wadogowadogo wa madini aina ya Rubi yaliyopo kijiji cha Kitwai A wilayani humo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Zephania Chaula.

  Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko akizungumza na mamia ya wachimbaji wadogowadogo wa madini katika mgodi wa madini ya Rubi uliopo katika kijiji cha Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara leo.
 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, Zephania Chaula akizungumza wakati wa mkutano baina ya Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko na Wachimbaji wadogowadogo wa madini katika mgodi wa madini ya Rubi uliopo katika kijiji cha Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara leo.
  Mhandisi Edward Joseph toka Tume ya Madini akijitambulisha  wakati wa mkutano baina ya Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko na Wachimbaji wadogowadogo wa madini katika mgodi wa madini ya Rubi uliopo katika kijiji cha Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara leo.

 Baadhi ya wananchi pamoja na wachimbaji wadogowadogo wakifuatilia mkutano baina yao na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko (hayupo pichani) kilichofanyika jana katika eneo la machimbo ya madini aina ya Rubi katika eneo la Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara leo.
 Mmoja ya wakazi wa kijiji cha Kitwai A, Alaiharwa Lenae akiwasilisha hoja kwa niaba ya jamii ya wafugaji mbele ya Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara kufuatia ziara ya Naibu Waziri huyo kutembelea eneo la mgodi wa uchimbaji madini ya Rubi uliopo katika kijiji hicho wilayani Simanjiro mkoani Manyara jana.
 Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko (kushoto) akitembea katika eneo la mgodi wa madini ya Rubi uliopo katika kijiji cha Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara jana. Naibu Waziri huyo amefanya ziara hiyo mgodini hapo kasha kuzungumza na wachimbaji wadogowadogo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu leseni za uchimbaji wa madini. Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Zephania Chaula na katikati ni mmoja wa wamiliki wa mgodi huo Raphael Mollel.
 Mmoja wa wamiliki wenye lesseni ya uchimbaji wa madini katika mgodi wa madini ya Rubi katika eneo la kijiji cha Kitwai A lililopo wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Raphael Mollel (kushoto) akielezea kuhusu upatikanaji wa madini hayo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko(watatu kutoka kulia) katika mgodi huo jana wilayani Simanjiro mkoani Manyara.Katika aliyeshika madini hayo ni Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Zephania Chaula.
 Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko (mwenye kofia ngumu) akitazama eneo ambalo linatumiwa kama lango la kuingilia ardhini katika mgodi wa kuchimba madini aina ya Rubi uliopo katika kijiji cha Kitwai A, Simanjiro mkoani Manyara aliotembelea eneo hilo jana.
 Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko (mwenye kofia ngumu) akisoma nyaraka za ukaguzi natathmini ya thamani ya madini wakati wa zziara yake katikamgodi wa uchimbaji wa madini yaina ya Rubi uliop kijiji cha Kitwai A wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara  alipotembelea eneo hilo jana. Kushoto ni mmoja wa wamiliki wa mgodi huo Raphael Mollel. (Picha na Idara ya Habari – MAELEZO, Simanjiro)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad