Mchezo wa kufuzu Mataifa Afrika (AFCON) 2019 nchini Cameroon baina ya Tmu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' na Cape Verde unaendelea hapa Uwanja wa Taifa.
Taifa Stars wanaongoza kwa goli mbili zilizofungwa na Mshambuliaji wa DifaaEl Jadida ya Morocco Saimon Msuva dakika ya 29 akipokea pasi ya Mshambuliaji wa GRC Genk Mbwana Samatta.
Mpaka Mapumziko Taifa Stars wanatoka kifua mbele kwa goli 1-0.
Katika kipindi cha Pili, Samatta anaipatia Taifa Stars goli la pili akimalizia pasi ya Mudathiri Yahya.
Taifa Stars walifanya mabadiliko ya kumtoa Abdi Banda na kuingia John Bocco, Mudathir nafasi yake ikichukuliwa na Feisal Toto
No comments:
Post a Comment