HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 18, 2018

SMARTPHONE, JEZI NA TIKETI KUTOLEWA KWA WASHINDI WA SHINDA ZAIDI NA SPORTPESA

Na Khadija Seif, Blogu ya Jamii
KAMPUNI ya mchezo wa kubashiri ya sportpesa  imechezesha droo   ya 28 ya promosheni ya shinda zaidi na sportpesa, ambapo Amri Nicolas(28) kutoka Kigoma ameibuka mshindi wa Bajaji RE.

akizungumza na vyombo vya habari Mkurugenzi wa utawala na udhibiti wa sportpesa Abass Tarimba ameeleza kuwa kuna  ongezeko kubwa la zawadi Kwenye promosheni hiyo. 

Tarimba ameeleza kuwa  wachezaji wa sportpesa kupitia mitandao yote wana nafasi ya kushinda  zawadi mpya .

Amesema kuwa  zawadi hizo zikiwemo smartphone, jezi za klabu ya Simba au Yanga pamoja na tiketi ya kuhudhuria mechi za ligi ya hispania na Uingereza kila mwezi.

Tarimba amesema kuwa  kutokana na ukubwa wa promosheni hiyo kwa sasa wameamua kuongeza zawadi zitakazotoka kila wiki na kila mwezi na
Ongezeko hilo la zawadi  limewekwa kwa lengo la kuhamasisha  wateja waweze kushiriki na kushinda zawadi mbalimbali kupitia mchezo huo wa kubashiri.

Amefafanua pia wateja waendelee kubashiri kwa wingi ili kujiweka Kwenye nafasi ya ushindi mnono ambapo unaweza kucheza kupitia mitandao yote, na mpaka sasa washindi kutoka Mikoa 13 wamepatikana ikiwemo Dar es salaam, Kigoma, Mwanza,Tanga, Singida, Ruvuma , Morogoro, Iringa, Kahama, Songwe, Mbeya, Pwani na Lindi. 
 Mkurugenzi wa utawala na udhibiti wa sportpesa Abass Tarimba(kulia) pamoja na  Mtangazaji wa Kipindi cha shinda  zaidi na SportPesa  Happiness Wandela(kushoto) wakionyesha Jezi ya Yanga kama zawadi kwa mshindi wa Promosheni ya Sinda na Sportpesa ambayo inatoa zawadi hizo zikiwemo smartphone, tiketi ya kuhudhuria mechi za ligi ya hispania na Uingereza kila mwezi.
 Mtangazaji wa Kipindi cha shinda  zaidi na SportPesa Happiness Wandela(kushoto) akizungumza na mmoja wa shindi wa shindano hilo leo. Kulia ni  Mkurugenzi wa utawala na udhibiti wa sportpesa Abass Tarimba

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad