Na Khadija Seif ,Globu ya Jamii
Msemaji wa timu ya Simba Haji Sunday Manara ametoa zawadi ya jezi pamoja na mipira kwa shule zote za Kata ya Tandale na kutoa wito kwa wazazi kutowanyima fursa watoto wao ambao wanavipaji ili kuwa mfano mzuri kama alivofanya msanii huyo Daimond Platinum .
Aidha amewapa taarifa rasmi atashirikiana bega kwa bega kwa wana michezo wa kata hiyo kuanzisha michuano ya Tandale Cup na kutoa fedha ya taslim kwa mshindi wa kwanza shilingi million 1, na kwa mshindi wa pili na watatu .
Manara ametoa fursa kwa Wanafunzi wa ulemavu wa ngozi pamoja na viungo kuwalipia ada mwakani kwa Wanafunzi watakaoingia kidato cha kwanza na darasa la kwanza.
No comments:
Post a Comment