HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 24, 2018

Europa League Mubashara ndani ya StarTimes

Katika mzunguko wa tatu wa ligi ya UEFA Europa, StarTimes kupitia chaneli ya World Football watakuwa wakiuonyesha mchezo wa Sporting CP dhidi ya Arsenal Mubashara majira ya Saa nne Usiku siku ya Alhamisi.
UEFA Europa League inafahamika kwa kuwa na ushindani wa hali ya juu lakini kuwa na matokeo yasiyotabirika kiurahisi. Mchezo wa Sporting CP na Arsenal unatarajiwa mkali sana hasa ukizingatia kiwango cha Arsenal kwa sasa, lakini pia kiwango kizuri cha miamba kutoka Ureno ambao wana faida ya kuchezea uwanja wao wa nyumbani wa Jose Alvalade.
Michezo mingine itakayopigwa usiku wa kesho na kuonyeshwa kupitia StarTimes ni RB Leipzig vs Celtic FC, Anderlecht vs Fenerbahce, AC Milan vs Real Betis, Olympic Marseille vs Lazio, pia Chelsea watakuwa nyumbani dhidi ya FC BATE Borisov. 
Kivutio kingine ni timu anayochezea Mtanzania Mbwana Ally Samatta, Genk ambayo itacheza ugenini dhidi ya Besiktas ya Uturuki. Mbwana Samatta amekuwa na kiwango kizuri sana akiichezea klabu yake lakini pia timu ya taifa ya Taifa Stars, wengi watapenda kumuona akiendeleza kiwango chake katika Usiku wa Europa dhidi ya Besiktas na sehemu pekee unapoweza kumuangalia ni kupitia king’amuzi cha StarTimes.
Mbali na ligi ya Europa, wikiendi hii ligi ya Ujerumani itaendelea kwa mechi kali kati ya RB Leipzig na Schalke 04 itakayochezwa saa 11:30 jioni siku ya Jumapili katika dimba la Red Bull Arena na Utarushwa LIVE na chaneli ya World Football ndani ya StarTimes tena kwa lugha ya Kiswahili.
Huko Ufaransa katika Ligue 1 kutakuwa na mchezo mwingine wa kukata na shoka ambapo mabingwa Paris Saint Germain watakuwa wageni wa Olympique Marseille katika uwanja wa Orange Velodrome. Mara ya mwisho walikutana mwezi wa pili ambapo Marseille walifungwa mabao 3-0. Marseille watamkosa mshambuliaji wao Florian Thauvan ambaye anauguza majeraha. Mchezo huo pia utaonyeshwa moja kwa moja kupitia World Football saa 5 Usiku siku ya Jumapili.
Burudani yote hii ya Soka inapatikana katika kifurushi cha MAMBO kwa watumiaji wa Antenna kwa Tsh 14,000 tu na kwa watumiaji wa Dish ni Tsh 21,000 kwa kifurushi cha SMART.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad