HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 4, 2018

YALIYOJIRI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akisisitiza jambo wakati wa kipindi cha maswali na majibu Bungeni jijini Dodoma.
 Mbunge wa Jimbo la Buyungu Mhe. Mhandisi Christopher Chiza akiapa mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job NdugaiS leo Jijini Dodoma mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimpongeza mbunge wa Buyungu Mhe. Mhandisi Christopher Chiza mara baada ya kula kiapo mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job  Ndugai leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akijibu swali Bungeni Kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuwezesha mikoa kutekeleza miradi ya kimkakati ya maendeleo ili kuinua uchumi wa mikoa hiyo.
 Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.  Dkt. Mary Mwanjelwa akieleza mikakati ya Serikali katika kuinua sekta ya kilimo hapa nchini wakati wa kipindi cha maswali na majibu leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Mbunge wa Kibakwe Mhe. George Simbachawene akisisitiza kuhusu faida za Dodoma kuwa makao makuu ya nchi yetu leo Bungeni  Jijini Dodoma.
 Sehemu ya wabunge wakifuatilia  mkutano wa 12 kikao cha kwanza cha Bunge leo Jijini Dodoma.(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad