HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 5, 2018

YALIYOJIRI BUNGENI LEO JIJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akizungumza na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma. Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge. Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akimsikiliza Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma. Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge. Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma, kwa Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge, Pia Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mbunge wa Muleba Kusini, Mhe. Anna Tibaijuka (kushoto) akiteta jambo na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu anaemuwakilisha Spika Ndugai, Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi wakimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kulia) wakati akiwashukuru Waheshimiwa kwa Kujitoa katika Shughuli Mbali mbali zinazohusiana na  Baraza hilo, moja wapo likiwa ni upimaji wa Virusi vya Ukimwi kwa hiari.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala Mhe. Mussa Zungu (katikati) anaemuwakilisha Spika Ndugai akikabidhiwa cheti kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kushoto) ikiwa ni Shukrani kwa Kujitoa kwao katika Shughuli Mbali mbali zilizoratibiwa na Baraza hilo, moja ya tukio likiwa ni upimaji wa Virusi vya Ukimwi kwa hiari, baada ya kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (mwenye tai nyeusi mbele), anaemuwakilisha Spika Ndugai akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Watendaji Wakuu kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), baada ya kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa na kulia kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kulia)


Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa (katikati) akizungumza na ugeni kutoka Ubalozi wa Marekani wanahusika na utekelezaji wa Miradi ya Ukimwi, Wajumbe wa kamati hiyo. Ugeni ulioongozwa na Mratibu Mkazi wa PEPFAR, Ndg. Brian Rettmann (kulia kwake) katika kikao kilichofanyika leo Bungenii Jijini Dodoma.
(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad