HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 14, 2018

WAZIRI MAHIGA AFUNGUA RASMI OFISI NDOGO ZA UWAKILISHI WA UBALOZI WA UJERUMANI JIJINI DODOMA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kwa pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Ofisi Ndogo ya Uwakilishi wa Ubalozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani jijini Dodoma. Ofisi hiyo ni ya kwanza kwa Balozi za nje zilizopo Tanzania kufunguliwa Dodoma. Ufunguzi huo ni katika kuitikia wito wa Mhe. Rais baada ya Serikali kuhamia rasmi Dodoma. Ofisi hizo ambazo zipo ghorofa ya nne katika Jengo la PSPF Barabara ya Benjamin Mkapa zitatoa huduma mbalimbali kwa Serikali, Bunge na Wananchi kwa ujumla huku zikisimamiwa na Bw. Richard Shaba ambaye ni Mtanzania. Pia Ofisi hizo zimejumuisha Mashirika ya Misaada ya Ujerumani ambayo ni GIZ na KFW.
Mhe. Waziri Mahiga kwa pamoja na Balozi Waechter wakifungua kitambaa kuashiria kuwa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zimefunguliwa rasmi jijini Dodoma
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo aliipongeza Serikali ya Ujerumani kwa uamuzi huo ambao ni ishara njema kwamba nchi hiyo inaunga mkono kwa dhati uamuzi wa Serikali wa kuhamia Dodoma. Pia alisema Tanzania ina mengi ya kujifunza kutoka Ujerumani kwani nchi hiyo ina uzoefu wa kuhamisha makao makuu kutoka Bonn kwenda Berlin ambapo ilifanya hivyo miaka 30 iliyopita
Mhe. Waziri Mahiga akiendelea na hotuba yake. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (wa nne kushoto), Balozi Waechter (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga (kushoto), Msimamizi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma, Bw. Richard Shaba (wa tatu kushoto), Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu (wa pili kushoto na Wawakilishi kutoka GIZ na KFW.
Mhe. Balozi Waechter nae akizungumza ambapo alisema wamefungua Ofisi hizo ili kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo katika nyanja mbalimbali kati ya Tanzania na Ujerumani

Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika picha na Mhe. Balozi Waechter pamoja na viongozi wengine walioshiriki hafla hiyo
Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Balozi Waechter ufunguzi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma
Wageni waalikwa walioshiriki ufunguzi wa Ofisi hizo wakifuatilia matukio mbalimbali
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na vyombo vya habari
Awali Mhe. Waziri Mahiga alisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zilizopo jijini Dodoma. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga
Mhe. Waziri Mahiga, Mhe. Balozi Waechter na Mkuu wa Dodoma Dkt. Mahenge wakiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa walioshiriki hafla hiyo wakiwemo Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Ujerumani nchini

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad