HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 4, 2018

UTPC:WAANDISHI SIYO MAADUI BALI NI WADAU WA MAENDELEO

 Rais wa Klabu za waandishi wa habari nchini Deogratius Nsokolo akizungumza katika mkutano wa UTPC unaofanyika Jijini Arusha katika ukumbu wa Lush Garden. Picha na Vero Ignatus.
 Mkurugenzi wa idara ya Maendeleo ubalozi wa Sweden Ulf Kallsting
 Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akizungumza na viongozi wa Klabu za waandishi wa habari kutoka mikoa tofauti hapa nchini. Picha na Vero Ignatus.
Afisa program, Mafunzo, Utafiti na Uchapishaji kutoka UTPC Victor Maleko akizungumza na viongizi wa Klabu za waandishi wa habari kwenye mkutano mkuu uliofanyika Mkoani Arusha.
 Mkurugenzi wa UTPC Abubakari Karsan akiwa na Mkuu wa idara ya Maendeleo ubalozi wa Sweden Na. Vero Ignatus. Arusha

RAIS wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Deogratius Nsokolo ameiomba serikali kuwaangalia waandishi wa habari kwa jicho la tofauti ili kuwalinda kwa kuwa tasnia hiyo sio adui bali ni wadau muhimu wa maendeleo ya Nchi.

Amesema hayo katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa wanachama wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania unaofanyika Jiini Arusha,ambapo amesema ndani ya miaka miwili waandishi 57 wamepata matatizo ya kupigwa,kuumizwa na kunyang'anywa vifaa vya kazi na baadhi kupote jambo ambalo linaleta woga katika utendaji kazi.

Nsokolo amesema hawawezi kutupia lawama kwa serikali kwa sababu hawajafanya uchunguzi wa kutosha,bali wanaomba kulindwa ili waweze kuchangia maendeleo kupitia kalamu zao.

''Napenda ifahamike pote kuwa waandishi wa habari sio maadui bali ni wadau muhimu wa maendeleo hivyo vema kushirikiana na sio kuonana maadui,"alisema

Aidha amemshauri Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Magufuli kuangalia aina ya viongozi anaowateua kutokana na hivi karibu kujitokeza hadharani baadhi ya kiongozi mmoja kutoa kauli tata kwa mwandishi wa habari aliyepigwa uwanja wa mpira Dar es Salaam.

"Ni wazi tukio hilo la kulaaniwa na halipaswi kufumbiwa macho tunaomba wahusika wachukuliwe hatua maana tunafahamu kabla ya kuingia uwanjani kuna kukaguliwa hivyo huwezi kuingia mtu na silaha,"alisema

Pia alisema katika mkutano huo iliohudhuriwa na wajumbe 81 toka Klabu 28 Tanzania Bara na Visiwani watatoa Tuzo ya tatu ya Daudi Mwangosi kama ishara ya kuonyesha waandishi hawako salama.

"Lakini tunaomba wafadhili wetu SIDA waangalie jinsi ya kusaidia Klabu ya Dodoma na tutapeleka andiko maalum ili wajengewe ofisi zenye hadhi kulingana na hali ilivyo sasa na kuwapatia mafunzo wanahabari ili wafahamu jinsi ya kuandika habari za viongozi mbalimbali wanaotembelea Dodoma,"alisema

Naye Mkuu wa Idara ya ushirikiano wa Balozi wa Sweden Tanzania (SIDA) Ulf Kastig alipongeza Klabu ya Arusha na Morogoro kubuni miradi kwa ajili ya kujiongezea kipato kwa ushirikiano na wadau wa mikoa yao.

Aliwakumbusha wanahabari kuhakikisha wanaandika habari za utafiti ili kuepuka kuleta shida katika nchi.

"Lakini ili Klabu zenu ziendelee kuwa na vyanzo vingi vya mapato vema mkaongeza idadi ya wanachama,"alisema

Alipongeza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Klabu za wanahabari na UTPC na kusema jambo la kuigwa kwani linajenga Demokrasia ya kweli.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro aliwaasa wanahabari kuzingatia maadili ya kazi zao licha ya kukabiliana na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa ajira.

Amesema Wilaya yake inakabiliwa na changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi ambayo sehemu kubwa inasabishwa na ukosefu wa uelewa wa sheria ya umiliki ardhi na baadhi ya wanasiasa kuitumia kujipatia kura.


"Mimi sitakubali kabisa kuachia wanasiasa wajinufaishe na migogoro hii lazima nibadilishe badala ya ardhi kuwalaana bali iwe baraka hasa Halmashauri ya Meru, na hili nimeanza kuzungumza na viongozi wadini tusaidiane kulimaliza," Picha na Vero Ignatus.

Kutoka katikati ni Rais wa RAIS wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Deogratius Nsokolo, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ubalozi wa Sweden Ulf Kallsting, wakwanza kushoto ni Kaimu mwenyekiti wa wa umoja wa Klabu za waandishi wa habari nchini Jane Mihanji. Picha na Vero Ignatus.
 Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Arusha Press Klab Cloud Ngwandu,akiwa na Katibu wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Arusha Mustafa Leu katika mkutano mkuu UTPC.


Na. Vero Ignatus. Arusha. 

RAIS wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Deogratius Nsokolo ameiomba serikali  kuwaangalia waandishi wa habari kwa jicho la tofauti ili kuwalinda kwa kuwa tasnia hiyo sio adui bali ni wadau muhimu wa maendeleo ya Nchi. 

Amesema hayo  katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa wanachama wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania unaofanyika Jiini Arusha,ambapo amesema ndani ya miaka miwili waandishi  57 wamepata matatizo ya kupigwa,kuumizwa na kunyang'anywa vifaa vya kazi na baadhi kupote jambo ambalo linaleta woga katika utendaji kazi.

Nsokolo amesema hawawezi kutupia lawama kwa serikali kwa sababu hawajafanya uchunguzi wa kutosha,bali wanaomba kulindwa ili waweze kuchangia maendeleo kupitia kalamu zao.

''Napenda ifahamike pote kuwa waandishi wa habari sio maadui bali ni wadau muhimu wa maendeleo hivyo vema kushirikiana na sio kuonana maadui,"alisema

Aidha amemshauri Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Magufuli kuangalia aina ya viongozi anaowateua kutokana na hivi karibu kujitokeza hadharani baadhi ya kiongozi mmoja kutoa kauli tata kwa mwandishi wa habari aliyepigwa uwanja wa mpira Dar es Salaam.

"Ni wazi tukio hilo la kulaaniwa na halipaswi kufumbiwa macho tunaomba wahusika wachukuliwe hatua maana tunafahamu kabla ya kuingia uwanjani kuna kukaguliwa hivyo huwezi kuingia mtu na silaha,"alisema

Pia alisema katika mkutano huo iliohudhuriwa na wajumbe 81 toka Klabu 28  Tanzania Bara na Visiwani watatoa Tuzo ya tatu ya Daudi Mwangosi kama ishara ya kuonyesha waandishi hawako salama.

"Lakini tunaomba wafadhili wetu SIDA waangalie jinsi ya kusaidia Klabu ya Dodoma na tutapeleka andiko maalum ili wajengewe ofisi zenye hadhi kulingana na hali ilivyo sasa na kuwapatia mafunzo wanahabari ili wafahamu jinsi ya kuandika habari za viongozi mbalimbali wanaotembelea Dodoma,"alisema

Naye Mkuu wa Idara ya ushirikiano wa Balozi wa Sweden Tanzania (SIDA) Ulf Kastig alipongeza Klabu ya Arusha na Morogoro kubuni miradi kwa ajili ya kujiongezea kipato kwa ushirikiano na wadau wa mikoa yao.

Aliwakumbusha wanahabari kuhakikisha wanaandika habari za utafiti ili kuepuka kuleta shida katika nchi.

"Lakini ili Klabu zenu ziendelee kuwa na vyanzo vingi vya mapato vema mkaongeza idadi ya wanachama,"alisema
Alipongeza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Klabu za wanahabari na UTPC na kusema jambo la kuigwa kwani linajenga Demokrasia ya kweli.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro aliwaasa wanahabari kuzingatia maadili ya kazi zao licha ya kukabiliana na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa ajira.

Amesema Wilaya yake inakabiliwa na changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi ambayo sehemu kubwa inasabishwa na ukosefu wa uelewa wa sheria ya umiliki ardhi na baadhi ya wanasiasa kuitumia kujipatia kura.

"Mimi sitakubali kabisa kuachia wanasiasa wajinufaishe na migogoro hii lazima nibadilishe badala ya ardhi kuwalaana bali iwe baraka hasa Halmashauri ya Meru, na hili nimeanza kuzungumza na viongozi wadini tusaidiane kulimaliza,"

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad