HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 5, 2018

Ujumbe Kutoka MCT Wakutana na Katibu Mkuu Wizara ya Habari jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Suzan Mlawi  akizungumza wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) na Baraza la Habari Tanazania (MCT),  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi akizungumza wakati wa kikao baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Suzan Mlawi(wapili kushoto) na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) pamoja na Baraza la Habari Tanazania (MCT),  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Kiongozi wa MCT, James Marenga, na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akipokea nyaraka yenye mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), Wallace Maugo(kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI)na MCT  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo hayo leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi, Rodney Thadeus, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa (katikati).
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akimsikiliza kwa makini kiongozi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), James Marenga (kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) na Baraza la Habari Tanazania (MCT),  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari –MAELEZO, Bibi. Zamaradi Kawawa, Mkurugenzi Msaidizi, Rodney Thadeus, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Rodney Thadeus akichangia mada wakati wa kikao baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(wanne kushoto) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Jumuiya ya Watetezi wa Haki za Kupata Taarifa na Baraza la Habari Tanazania (MCT),  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akimsikiliza kwa makini Mjumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI), Dkt. Samwilu Mwafisi (kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa muunganiko huo na Baraza la Habari Tanazania (MCT),  walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa, Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo na Kiongozi wa MCT, James Marenga.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) pamoja na Baraza la Habari Tanzania (MCT) mara baada ya kumaliza kikao leo Jijini Dodoma. Waliokaa kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya MCT, Wallace Maugo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicolas William Mkapa, na Mshauri wa Mradi wa Ufuatiliaji wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOM), Dkt. Samwilu Mwafisi. (Picha na: Idara ya Habari – MAELEZO).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad