HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 5, 2018

TMA kupunguza athali zitokanazo mabadiliko ya hali ya hewa kwa wananchi

Na Karama Kenyunko, Blogu ya Jamii.
MAMLAKA  ya Hali ya Hewa nchini (TMA) leo Septemba 5, 2018 imesema tathmini inaonesha kuwa kwa sasa wananchi wengi wamepata uelewa mkubwa wa hali ya hewa hali ambayo inatarajiwa kupunguza athari zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa kwa wananchi kuchukua hatua stahiki katika kupunguza majanga.

Imeelezwa kuwa, tathimini zinaonyesha kuwa wananchi wamekuwa wakifatilia sana utabiri wa hali ya hewa kuliko miaka ya nyuma  kutokana na kuwepo kwa viwango sahihi. Vinavyotolea na TMA.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa  warsha ya wanahabari kuhusu utabiri wa mvua za msimu wa vuli za Otoba mpaka Desemba 2018, jijini  Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt Agnes Kijazi amesema, usambazwaji wa taarifa za hali ya hewa unaofanywa na vyombo mbali mbali vya habari juu zimewezakusaidia kuongeza uelewa kwa wananchi, na mpaka sasa wengi wamekuwa wakifuatilia utabiri huo na kuutumia ipasavyo.

Taarifa ya hali ya hewa taarifa ya hewa ni muhimu sana kwa jamii katika kila sekta mbali mbali ka vule ya Kilimo, afya, miundombinu na zinginezo hasa katika wakati huu wa kuelekea kuwa na uchumi wa viwanda.

"Taarifa za hali ya hewa ni muhimu sana kwa Jamii katika kila sekta, ukizungumzia uchumi wa viwanda lazima utahitaji taarifa za hali ya hewa na hata katika katika sekta zingine zote kama vile, Kilimo,Afya,Mifugo,Nishati,Usafiri wa anga,usafiri wa kwenye maji usafiri wa nchi kavu ,Utalii na Maliasili, elimu na sekta nyingine nyingi."amesema Dkt Kijazi.

Alisema utabiri unaotolewa unasaidia wananchi kuchukua hatua stahiki ili kupunguza athari zinazotarajiwa ikiwemo mafuliko na kusaidia wakulima katika kufanya shughuli zao za kilimo.

Dkt Kijazi alisema Wananchi wengi kwa sasa  wanafahamu na kufatilia utabiri wa hali ya hewa kwa sababu unawasaidia katika shughuli zao.
Dkt Kijazi amesema utabiri wa msimu wa mvua za vuli, Oktoba-Desemba 2018 utatolewa kesho.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, (TMA), Dkt Agnes Kijazi (katikati) akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya wanahabari kuhusu utabiri wa mvua za msimu za Vuli, Oktoba hadi  Desemba 2018 iliyofanyika leo katika Ofisa za mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Utabiri wa TMA Samwel Mbuya na  kushoto kwake ni Hellena Msemo, Meneja utendaji.
Wanahabari wakifuatilia kwa makini mada juu ya utabiri wa hali ya hewa kwa msimu wa mvua za Vuli za Oktoba hadi Desemba 2018.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, (TMA), Dkt Agnes Kijazi akiwa kwenye picha ya pamoja na waandishi wa habari leo kwenye ufunguzi wa  warsha ya wanahabari kuhusu utabiri wa mvua za msimu wa vuli za Otoba mpaka Desemba 2018, jijini  Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad