HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 6, 2018

TBA WAKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA BUNJU, WANANCHI WAKARIBISHWA KUZINUNUA

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh. Elias Kwandikwa amefanya ziara katika mradi wa nyumba zinazojengwa kupitia wakala wa majengo nchini (TBA) katika eneo la Bunju jijini Dar es salaam na kushauri wanananchi kujitokeza kununua nyumba hizo.

Akiongea baada ya kukagua nyumba hizo Kwandikwa amesema kuwa amekagua mradi huo na kuridhishwa na unavyoendelea kwa kuwa hadi sasa nyumba 279 kati ya nyumba 851 ambazo zipo kwenye malengo zimekamilika.

Kwandikwa amesema kuwa wananchi na wafanyakazi wajitokeze kununua nyumba hizo na kama serikali wanasimamia ili waweze kupata kilicho bora.

Aidha ameeleza kuwa heka 650 zilizopo Dodoma zitaanza kufanyiwa mradi huo mapema ili kuweza kuongeza makazi ya kutosha jijini humu katika wakati huu ambapo idara nyingi zimehamia Dodoma.

Pia amewataka wakala wa majengo nchini kutoa matangazo ili wananchi wajue kuna nyumba nzuri na bora zilizokamilika ili waweze kununua.

Na amewataka wafanyakazi wa wakala hiyo kufanya kazi kwa weledi na amewashauri waharakishe mradi wa ujenzi wa nyumba Dodoma.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TBA  Idara ya miliki Baltazari Kimangano ameeleza kuwa kuna nyumba za viwango vyote  na hadi sasa nyumba 105 zimekamilika  na wateja bado wanauhitaji na kwa wafanyakazi wanaweza kulipia miaka 7 kwa nyumba hizo.

Pia amesema kuwa wateja wanaweza kupata mikopo kupitia benki za CRDB, NBC, BOA na wanamazungumzo na benki ya Zanzibar ambazo zitatoa mkopo kwa riba nafuu kwa wateja wao ili kuweza kupata nyumba hizo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Mh. Elias Kwandikwa (katikati)akiwa na viongozi wa wakala wa majengo nchini (TBA) wakati alipofanya ziara ya kukagua nyumba za umma zilizojengwa na TBA zilizokamilika huko Bunju.
 Mkurugenzi wa Idara ya umiliki wa  mamlaka ya majengo nchini Bartazari Kimangano (kushoto) akimuongoza naibu waziri kukagua baadhi ya nyumba hizo.
Baadhi ya nyumba  zijulikanazo kama Villa ambazo zimekamilika na zipo tayari kwa makazi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad