HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 12, 2018

NAIBU WAZIRI MHANDISI NDITIYE AZINDUA WIKI YA SHIRIKA LA RELI NCHINI

Na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii
Naibu Waziri wa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiy amefungua wiki ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) pamoja na kuzindua nembo na kuzindua nembo mpya ya shirika hilo.

Akizungumza na waaandishi  wa habari leo jijini Dar es Salaam Mhandisi Nditiye amesema juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano  kupitia ilani ya CCM katika sekta ya usafirishaji zitapelekea kuondoa kero mbalimbali na kukuza vipato vya wananchi

Mhandisi Nditiye amesema ili huhakikisha kauli mbiu ya uchumi wa viwanda inatekelezwa kwa ufanisi kwa kutumia miundombinu ya reli ya kisasa na uboreshaji wa reli ya kati kuelekea Dar -Isaka.
Mhandisi amesema juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa wananchi wa Tanzania tushirikiane kwa pamoja kuunga mkono juhudi za serikali inayoongozwa na Mh.Rais Dkt.John Joseph Pombe Magufuli.

"Nawahakikishi kuwa serikali ya awamu tano itaendelea kuboreha huduma kwa wananchi na kuimarisha miundombinu ya reli na yenye lengo la kuleta manufaa na maendeleo ya Taifa la leo na kesho,"alisema Mhandisi Nditiye
 Mwenyekiti wa bodi ta Wakurugenzi Shirika la Reli Tanzania (TRC),Profesa John Wajanga akizungumza waandishi wa habari katika ufunguzi wa wiki ya Shulilika la reli Tanzania leo hadi September 15 mwaka huu.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza leo na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa wiki ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) na  kuwapongeza kwa nzuri na kusimamia vema shunguli za miradi mbalimbali inayoendelea ikiwemo wa ujenzi wa reli.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa bodi ta Wakurugenzi Shirika la Reli Tanzania (TRC),Profesa John Wajanga (picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (wa tatu kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa wiki ya Shirika la reli Tanzania.
Meneja Uhusiano shirika la Reli Tanzania-TRC,Jamila Mbarouk akifafanua jambo katika ufunguzi wa shirika la Reli Tanzania.
 Wanafanyakazi wa shirika la Reli Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad