HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 3, 2018

MAADHIMISHO YA WAHANDISI TANZANIA KUFANYIKA AGOSTI 5-7, UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wahandisi Tanzania, Mhandisi Ngwisa Mpembe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana naMaadhimisho ya Siku ya Wahandisi hapa nchini Bodi ya Usajili Wahandisi nchini.
 Kaimu Msajili toka Bodi ya Usajili Wahandisi (ERB), Mhandisi Patrick Barozi (kulia) akionesha kwa waandishi wa habari picha za wahandisi waliokuwepo kipindi cha uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1968 wakati akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam leo.
  Kaimu Msajili toka Bodi ya Usajili Wahandisi (ERB), Mhandisi Patrick Barozi (kulia) akionesha kwa waandishi wa habari hati iliyosainiwa na Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere mwaka 1968 ili kuanzishwa kwa bodi hiyo, kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wahandisi Tanzania, Mhandisi Ngwisa Mpembe.
Msajili Msaidizi wa Bodi ya usajili wa Wahandisi (Kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

BODI ya usajili ya wahandisi kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake pia wahandisi wataalam watakula kiapo cha utii, Maadhimisho hayo  yatafanyika katika ukumbi wa DiamonJubilee jijini Dar es Salaam kuanzia Agosti 5 hadi 7.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mhandisi Ngwisa Mpembe amesema kuwa Jumuiya ya wahandisi nchini, taasisi na mashirika ya kihandisi, jamii ya wafanyabiashara pamoja na jamii kwa ujumla kuwa siku ya wahandisi Tanzania itaadhimishwa Agosti 5-7.


"Siku ya wahandisi ni siku pekee kwa wahandisi wa Tanzania kuweza kuonyesha yale wanayoweza kufanya kwa maendeleo ya taifa". Amesema Mhandisi Mpembe.

Amesema kuwa  maadhimisho hayo shughuli mbalimbali zitafanyika kama majadiliano ya kitaaluma, kiapo cha wahandisinwatalaam, maonyesho mbalimbali ya kiufundi na biashara, kutoa tuzo kwa wahandisi na waliosaidia uhandisi ndani ya miaka 50, kutambua na kuzawadia na kuwatambua wahitimu waliofanya vizuri zaidi katika mitihani yao ya mwaka wa mwisho wa masomo 2017/2018.

Maadhimisho ya siku ya wahandisi Tanzania 2018 inafanyika kila mwaka na mwaka huu ni mwaka wa sita tangu kuanzishwa kwake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad