HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 2, 2018

Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Leo limeadhimisha miaka 54 tangu kuanzishwa kwake

Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Leo limeadhimisha miaka 54  tangu kuanzishwa kwake.

Maadhimisho hayo yamefanyika jijini Dar es salaam chini ya Mkuu wa Majeshi Generali Venance Mabeyo akiwa na mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, kwa kufanya usafi katika eneo la kambi ya Jeshi Lugola na  baadaye kufuatiwa na michezo iliyofanyika katika eneo la Uwanja wa Jeshi mwenge vinyago .

Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amelipongeza Jeshi hilo kwa kudumisha usafi na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuiga mfano wa Jeshihilo kutumia mazingira kwa usafi na kupanda miti katika maeneoyao.

Aidha Makonda ameelezeakusikitishwa kwake na kitendo cha mgambo wanaosimamia usafi katika jijini la Dar es salaam kwenda kinyume cha sheria katika kusimamia zoezi hilo kwakupiga wananchi na kusema kuwa hajawatuma kufanya hayo  na ametoa amri wakamatwe .

''Sheria zipo hakuna hata mmoja inayosema adhabu ya kukutwa na uchafu ni kupigwa bali sheria imeongelea faini, nimeagiza tangu jana walihusika na hilo tukio wakamatwe na hatua za sheria zichukuliwe dhidi yao" alisema. 

Kwa upande wake mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo amewataka wanajeshi kudhibiti usalama wa kambi  kwa kutoruhusu raia kukatisha  katika maeneo ya Jeshi  na kuahidi kujenga ukuta katika eneo la jeshi kambi ya Lugalo na  Mwenge na kuhiza usafi kuwa endelevu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda paulo makonda akiwa ameambatana na Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Tanzania jenerali, Venance wakiwasalimi wachezaji wa tumi moja ikiwa ni ya Jeshe na moja siyo ya jeshi katika maazimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
 Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Tanzania jenerali,Venance Mabeyo akizungumza viongozi mbalimbali pamoja na wanajeshi la JWTZ  katika maazimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwake.
 Mbwa wa jeshi akizibiti adui
 Mbwa wa jeshi akizibiti adu alie kua akirukuka ukuta


Michezo ikiendelea katika uwaja jeshi  Mwenge jijini Dar as Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad