HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 6, 2018

CHAMA CHA WABUNGE MARAFIKI WA UTURUKI WAKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA UTURUKI NCHINI TANZANIA, BUNGENI JIJINI DODOMA

 Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Fatma Toufiq (kulia) akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (katikati) kwa lengo la kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto ni Mwandishi Mwandamizi wa Taarifa Rasmi za Bunge, Ndg. Patson Sobha
 Wajumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki wakiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Fatma Toufiq (watatu kushoto) wakimsikiliza Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (wa pili kushoto) wakati wa kikao baina yao kilicholenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma.
 Wajumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki wakiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Fatma Toufiq (katikati) wakiwa katika mazungumzo na  Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (wa pili kushoto) wakati wa kikao baina yao kilicholenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (kulia) akizungumza na Wanachama wa  Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki walioongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Fatma Toufiq (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kililenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi
Mjumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki na Mbunge wa Chilonwa, Mhe. Joel Mwaka akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu na Wanachama wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki (hayupo kwenye picha) katika kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad