HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 2, 2018

Urasimishaji Biashara Waingiza Mapato Zaidi ya Milioni 600 Manispaa ya Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Kebwe Steven Kebwe akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njolay alipofika ofisi kwa Mkuu wa Mkoa huyo hivi karibuni mjini Morogoro. Kutoka kulia ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Kapteni mstaafu John Chiligati, Mtendaji Mkuu wa MKURABITA, Bibi. Seraphia Mgembe na mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA Bw. Emmanuel Mayeji.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Cliford Tandari akiteta jambo na wajumbe Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) pamoja na watendaji wa mpango huo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Balozi Daniel Ole Njolay (katikati) walipotembelea ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro hivi karibuni. Kutoka kulia ni mjumbe wa Kamati hiyo Emmanuel Mayeji, Mtendaji Mkuu wa MKURABITA, Bibi. Seraphia Mgembe, Mwenyekiti mstaafu wa kamati hiyo Kapteni John Chiligati na mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo, Bw. Ibrahim Janabi.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogorgo, Bi. Ruth John akielezea jambo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) pamoja na watendaji wa mpango huo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Balozi Daniel Ole Njolay (katikati) walipotembelea ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Morogoro hivi karibuni.
Mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Bibi. Anna Mwasha aakifafanua jambo mbele ya Afisa Biashara wa Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Mratibu wa MKURABITA katika Manispaa hiyo, Bw. Herman Festus wakati wa ziara ya kutembelea Kituo Kimoja cha Urasimishaji na Uendelezaji wa Biashara  katika Manispaa ya Morogoro hivi karibuni.Kituo hicho kinatoa huduma za urasimishaji wa biashara ambapo mpaka sasa kimefanikiwa kurasimisha biashara 5000 na kufanyikisha ukusanyaji wa mapato ya takribani shilingi milioni 500. Kulia kwake ni Meneja wa Urasimishaji wa Biashara Heavy Kombe na mmoja wa watoa huduma wa Kituo hicho Bi. Mary Lyimo.
Mtendaji Mkuu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA),Bibi. Seraphia Mgembe akijadili jambo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Wanawake Wazalishaji wa Chakula Tanzania (WFPT), Bibi. Emmy Kiula hivi karibuni mjini Morogoro. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njolay.
Mtendaji Mkuu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA),Bibi. Seraphia Mgembe akikagua kifungashio cha mvinyo walipotembelea Kampuni ya ADUKE Food Processing wakati wa wa ziara ya kutembelea wanufaika wa mafunzo ya MKURABITA mkoani Morogorogo hivi karibuni. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njolay, kushoto ni Afisa Biashara Manispaa ya Morogoro, Herman Festus na wapili kushoto ni mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA Bibi. Angelista Kihaga.
Mwenyekit wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njolay akiongoza kikao cha majumuisho baada ya kuhitimisha ziara ya siku 12 kukagua maendeleo ya utekelezaji ya shughuli za Urasimishaji Ardhi na Biashara katika maeneo ya Urambo, Bariadi, Ikungi, Chamwino na Manispaa ya Morogoro kikoao kilichofanyika mjini Morogoro mapema hivi karibuni. Picha na Frank Shija- MAELEZO

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad