HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 25, 2018

ZIARA YA WAZIRI KANGI LUGOLA KATIKA KITUO CHA POLISI MURIET JIJINI ARUSHA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na wananchi wa Kata ya Muriet, baada ya kutembelea Kituo cha Polisi na nyumba za askari polisi zilizopo eneo hilo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (kulia) na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’anzi (kushoto) kutembelea Kituo cha Polisi cha Muriet (kinachoonekana pichani) na nyumba za askari polisi zilizopo katika eneo hilo wakati wa ziara yake jijini Arusha. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiangalia pikipiki zilizotolewa na wadau wa kupinga vita uhalifu kwa Kituo cha Polisi Muriet, kilichopo Kata ya Muriet. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’anzi.Waziri Lugola yupo jijini Arusha kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola(wapili kushoto), alipotembelea nyumba za askari polisi zinazoonekana pichani, katika eneo la Kata ya Muriet,jijini Arusha.Kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,Ramadhani Ng’anzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad