HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 5, 2018

Wafanyakazi wa NEMC wafikishwa Kizimbani

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Wafanyakazi wa  NEMC na wenzao  wamefikishwa katika ma ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka nane ya uhujumu uchumi likiwemo la kughushi saini ya Waziri wa nchi ofisi ya makamo wa rais muungano na Mazingira,Januari  Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa Mazingira.

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao jana Julai 4/2018 na wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga  mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Maira Kasonde.

Washtakiwa  wametajwa kuwa ni Afisa wa Mazingira NEMC, Deusdith Bulamire (38) Mkazi wa Ubungo, Edna Lutanjuka, Sekretari wa Nemc,  Mwaruka Mwaruka (42) Mkazi wa Ukonga Mombasa na Mkaguzi kutoka ofisini ya CAG, Dauson Barwongeza Mkazi wa Dodoma.

Akisoma hati ya mashtaka wakili Katuga amedai kati ya Machi 28,2017 na Novemba 4,2018 Dar es Salaam washtakiwa walikula njama ya kutenda kosa la kughushi.

Washtakiwa Deusdith, Edna na Mwarukwa wanadaiwa, Oktoba 10,2017 Dar es Salaam kwa udanganyifu walighushi cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3366 wakijaribu kuonesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewana NEMC wakati wakijua si kweli.

Washtakiwa hao, pia wanadaiwa kughushi cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira chenye usajili namba EC/ EIA/3365 wakijaribu kuonesha cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati wakati wakijua si kweli.

Pia wanadaiwa kughushi saini ya Waziri Makamba kwenye cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira wakijaribu kuonesha sahihi hiyo ni ya Waziri huyo wakati si kweli.

Katika shtaka la tano washtakiwa Deusdith, Edna na Mwarukwa walighushi saini ya Waziri Makamba katika cheti cha tathmini ya uharibifu wa mazingira wakijaribu kuonesha sahihi hiyo ni ya  Waziri huyo wakati si kweli.

Katika shtaka la sita mshtakiwa Edna anadaiwa kuwa Novemba 2017 katika ofisi za NEMC Makao Makuu Dar es Salaam kwa kujua alitoa cheti cha kughushi cha tathmini ya uharibifu wa mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3365 cha Oktoba 16,2017 kwa E 2598 D/CPL David wakijaribu kuonesha ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC.

Katika shtaka la saba, imedaiwa kuwa kati ya Machi 28 na Novemba 4,2017  washtakiwa hao walijipatia sh. milioni 30 kutoka kwa F1195 CPL Yohana Mtweve kwa kudai kuwa wangeweza kufanya tathimini ya uharibifu wa mazingira na kumpatia cheti ambacho kinatolewa na NEMC huku wakijua kuwa si kweli.

Washtakiwa hao pia wanadaiwa kuwa kuisababishia NEMC hasara ya Sh milioni 20.

Washtakiwa hao hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Kwa mujibu wa upande  mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Washtakiwa wamepelekwa rumande hadi Julai 18,2018 kwa ajili ya kutajwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad