Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Mhe. Dkt.
John Pombe Magufuli anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kidunia wa Vyama vya Siasa
(Mkutano maalum kwa Kanda ya Afrika) uliondaliwa na Chama cha Kikomonisti cha
Watu wa China (CPC).
Akizungumza
na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi
wa CCM, Humphrey Polepole amesema kuwa Mkutano huo utakao husisha Vyama 40 utakuwa
wa kwanza kufanyika nje ya China na wa pili baada ya ule wa uliofanyika China.
Polepole
amesema ni heshima kubwa kwa Serikali ya Tanzania, Nchi na Chama cha Mapinduzi (CCM)
kutokana na Mkutano huo kuhusisha pia washiriki zaidi ya 200 kutoka Afrika na
nje ya Afrika.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa
Uhusiano wa Afrika (IDCPC), Wang Heming amesema kuwa Mkutano huo unafanyika
Tanzania ni kutoka ushirikiano mzuri ulikuwepo baina ya China na Tanzania, pia
Tanzania ni nchi ambayo imehusika katika Ukombozi wa Bara la Afrika.
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika siku mbili ambapo utafunguliwa na Rais Magufuli, kesho Julai 17 na kufungwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi atakayemuwakilisha Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu mkutano wa kidunia wa vyama kiaiasa vya Barani Afika kwa ushirikiano na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC). Kushoto ni Mkurugenzi wa wa Mawasiliano kwa Umma, Sun Haiyan na kulia ni Naibu Mkurugenzi mkuu wa Uhusiano wa Afrika (IDCPC) Wang Heming.
Mkurugenzi wa wa Mawasiliano kwa Umma, Sun Haiyan(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu mkutano wa vyama vya siasa vipavyo 38 vilivyofika kuudhuria mkutano huo utakaofanyika kesho katika ukumbi wa hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment