Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Makani
Makwaia akikaribisha timu ya wataalamu kutoka China ambao wamekuja
kujenga uwezo kwa wataalamu wa hapa nchini na kusaidia maeneo ambayo yana upungu
wa wataalamu Muhimbili, Taasisi ya Mifupa MOI, Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Rufaa ya Mbeya. Kutoka kushoto ni
viongozi wa watalaamu hao na kulia ni Mkurungezi Mtendaji wa JKCI, Prof.
Mohamed Janabi na anayefuatia ni mwakilishi wa MOI, Dkt. Swai. Leo
Muhimbili, MOI na JKCI imewaaga wataalamu watatu ambao walikuwa hapa
nchini. Tanzania na China imekuwa ikishinikiana kwa zaidi ya miaka 50
katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwamo sekta ya afya.
Wataalamu kutoka China ambao watashirikiana na wataalamu
wetu wa MNH, MOI, JKCI na Hospitali ta Rufaa ya Mkoa Mbeya katika kutoa
huduma za kitabibu. Miongoni mwa kundi hilo wamo wataalamu watatu; Dkt.
Zhu Jian, Dkt.Wang Qiang na Song Tao ambao wameagwa leo baada ya
kumaliza muda wao.
Mwakilishi kutoka MOI akizungumza na wataalamu kutoka China
ambao wamekuja kujenga uwezo kwa wataalamu wa hapa nchini na kusaidia maeneo ambayo yana upungu wa wataalamu Muhimbili
ambao wamekuja kujenga uwezo kwa wataalamu wa hapa nchini na kusaidia maeneo ambayo yana upungu wa wataalamu Muhimbili
Mkurungezi Mtendaji wa JKCI, Prof. Mohamed Janabi akiwakaribisha watalaamu hao kutoka China ambao wamekuja
kujenga uwezo kwa wataalamu wa hapa nchini na kusaidia maeneo ambayo yana upungu
wa wataalamu Muhimbili
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Makani
Makwaia akimpatia cheti Dkt. Zhu Jian ambaye amemaliza muda wake.
Dkt. Wang Qiang akionyesha cheti chake baada ya kupewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji.
Mwakilishi wa MOI, Dkt. Swai akimuaga Song Tao ambaye pia amemaliza muda wake nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Bw. Makwaia akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu hao na watumishi wa taasisi tatu ambazo ni MOI, JKCI na Hospitali ya Taifa Muhimbili.
No comments:
Post a Comment