HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 13, 2018

RAIS DK.SHEIN AWAFUTARISHA WANANCHI MKOA WA MJINI MAGHARIBI UNGUJA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipojumuika na Viongozi na Wananchi wa  Mkoa wa Mjini Magharibi  katika Futari aliyowaandalia jana katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar  ikiwa ni mwendelezo wake wa kufutarisha kila ifikapo kipindi kama hichi,(kulia) Rais mstaafu wa Zanzibar Dkt.Amani Abeid Karume
 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (katikati) akijumuika na Viongozi Wanawake na Wananchi wengine katika Futari aliyoandaliwa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar jana
  Baadhi ya Akinamama wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika Futari iliyoandaliwa jana na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar katika  mwendelezo wake wa kuwafutarisha Wananchi hao kila ifikapo Mwezi 27 wa Mfungo wa Ramadhan
 Wananchi na Waislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika Futari iliyoandaliwa jana na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar ikiwa ni mwendeleo wake kila ifikapo mwezi 2y ya Mfungo wa Ramadhan kuwafutarisha Wananchi 
 Kadhi Mkuu wa Zanzibar  Sheikh Khamis Haji (kulia) alipokuwa akisoma Dua kumuombea Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) baada ya futari aliyoiandaa kwa Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar, ikiwa ni mwendelezo wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa Mikoa huo 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiagana na Wananchi mbali mbali  waliohudhuria katika Futari iliyowaandalia Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi jana  katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar ikiwa ni katika mpangilio wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa  Mikoa huo kila ifikapo mwezi 27 ya Mfungo wa Ramadhan


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad