HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 21, 2018

NAIBU WAZIRI NDITIYE AITAKA TAA KULIPA FIDIA

 Mkurugenzi Uendelezaji Miliki wa Shirika la Nyumba (NHC), Hakimeni Mlekio, akieleza hatua ya upanuzi wa jengo la abiria katika kiwanja cha ndege cha Dodoma kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (wa tatu kulia), wakati Naibu Waziri huyo alipokagua maendeleo ya mradi huo. Kukamilika kwa upanuzi wa jengo hilo kutaongeza idadi ya namba ya abiria 35 mpaka 145.
 Meneja wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), mkoani Dodoma, Ludovick Ndumbaro akimweleza Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia), matumizi ya taa za kuongozea ndege kiwanjani hapo, wakati Naibu Waziri huyo alipokagua maendeleo ya mradi huo. Katikati ni Meneja wa Kiwanja hicho, Bertha Bankwa.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, akizungumza na  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Richard Mayongela (kulia), pamoja na uongozi wa TAA, TCAA na TMA mkoa wa Dodoma, mara ya kukagua maendeleo ya upanuzi wa jengo la abiria katika kiwanja cha Ndege cha Dodoma.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, akitoa maelekezo kwa uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), mkoa wa Dodoma, mara baada ya kukagua karakana ya shirika hilo jijini hapo. Kushoto ni Mkuu wa Stesheni, Bi. Rose Ngauga.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, akizungumza na watumishi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) mkoa wa Dodoma, mara baada ya kukagua karakana ya shirika hilo jijini humo.
 Watumishi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (hayupo pichani), wakati Naibu Waziri huyo alipozumgumza nao mara baada ya kukagua karakana ya shirika hilo jijini Dodoma.Kushoto ni Stesheni masta, Bi. Rose Ngauga.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, akizungumza na Maafisa  wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) mkoani Dodoma, mara baada ya kutembelea ofisi ya mamlaka hiyo. Kushoto ni Afisa Mfawidhi Konrad Shio.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad