HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 1, 2018

MKUU WA MAGEREZA NCHINI SHELISHELI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA JIJINI DAR

 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa akisalimiana na Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange ofisini kwake alipowasili Makao Makuu ya Magereza leo Juni 1, 2018 katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili.
 Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiongoza mazungumzo Ofsini kwake  na Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange(hayupo pichani), leo Juni 1, 2018 alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.
 Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange akitambulisha ujumbe wake alioongozananao(hawapo piachani) kabla ya utilianaji saini makubaliano ya ushirikiano na Jeshi la Magereza.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) akisaini Mkataba  wa makubaliano ya ushirikiano baina ya Magereza nchini SheliSheli na Jeshi la Magereza Tanzania Bara. Kushoto ni Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli hiyo Raymond St Ange akisaini mkataba huo.  Hafla fupi ya  utilianaji saini Mkataba huo umefanyika leo Juni, 2018 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) na Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange wakionesha nyaraka za Mkataba wa makubaliano mara baada ya utiliananji wa mkataba huo ambapo Jeshi la Magereza linatarajia kupeleka baadhi ya Maofisa wa Jeshi hilo kwenda nchini SheliSheli kusaidia kuwajengea uwezo wa Uendeshaji wa Magereza nchini humo.
 Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakishuhudia utiliananji saini wa mkataba huo (Kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(katikati) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila Kushoto ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Charles Novart.
  Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange(kushoto) akiwa pamoja na ujumbe wake  kabla ya kusainiana Mkataba wa makubaliano hayo,(kulia) ni Balozi wa Heshima wa SheliSheli nchini Tanzania, Maryvonne Pool akifuatilia mazungumzo hayo kama inavyoonekana katika picha.
 Mkuu wa Magereza Mkoani Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Magereza, Augustine Mboje(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange alipowasili katika Gereza Kuu Ukonga, Dar es Salaam kutembelea Kiwanda cha Useremala na ushonaji leo Juni 1, 2018.
 Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange pamoja na ujumbe wake na Maofisa wa Jeshi la Magereza wakitembezwa ndani ya Kiwanda cha USeremala  Gereza Kuu Ukonga kama inavyoonekana katika picha.
 Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange akitosi dafu na Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga kabla ya kupata chakula cha mchana mara baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam.
 Kamishna Jenerali wa Maagereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Magereza nchini SheliSheli, Raymond St Ange(wa tatu kushoto) walioketi, (wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga, (wa pili toka kushoto) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila,(wa tatu toka kulia) ni Balozi wa Heshima wa SheliSheli nchini Tanzania, Maryvonne Pool. Wengine waliosimama mstari wa nyuma ni Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza pamoja na Maofisa kutoka nchini SheliSheli(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad