Na Agnes Francis,Glob ya jamii
WAKAZI wa Kanda ya Ziwa wamejikuta wakishuhudia burudani ya aina yake kutokana na kushuhudia mchezo wa mashindano ya pikipiki.
Burudani hiyo ya aina yake ambayo ni sehemu ya kusheherekea Sikukuu ya Eid imeandaliwa na Tamasha la Sport Music Festival.
Hivyo kwa leo tamasha hilo kinaendelea kufanyika katika Mkoa wa Geita wakati wa kusherehekea Sikukuu ya Eid.
Wananchi wa Mkoa huo tangu mapema wamejitokeza kwenye tamasha hilo na mchezo wa pikipiki ilikuwa kivutio kikubwa kutokana na umahiri waliokuwa wanaendesha pikipiki hizo.
Wengi wao waliwathibitishia wakazi waliofika kwenye tamasha hilo kuwa wanajua vema kuchezea pikipiki hali iliyosababisha kuibua shangwe.
Baada ya michezo ya pikipiki usiku huu wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanaaanda kupanda jukwaani kutoa burudani kwa mashabiki wa muziki huo.
Ambapo pia wasanii wa kizazi kipya watakuwepo kutoa katika kuendeleza sherehe hizo.
Wakati wa kusherekea sikukuu ya Idd kwa wakazi wa Geita walishuhudia michezo ya pikipiki iliyokuwa ikitoa burudani uwanjani hapo.
Mmoja wa vijana akionesha umahili wa kuchezesha baiskeli wakati wa sherehe za Idd zilizofanyika Geita
Baadhi ya wananchi wa Geita wakifuatilia burudani ya baiskeli, pikipiki na magari ikiwa ni sehemu ya kusheherekea Sikukuu ya Eid imeandaliwa na Tamasha la Sport Music Festiva
No comments:
Post a Comment