HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 9, 2018

MABULA AHAKIKI UHAWILISHAJI ARDHI KATIKA VIJIJI VYA NAKAWALE NA LILAHI PERAMIHO HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA RUVUMA

 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma alipoanza  ziara yake ya siku mbili kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi na kuhakiki uhawilishaji wa ardhi ya kijiji mkoani humo.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akihakiki majina katika kijiji cha Nakawale halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wakati wa ziara yake ya kuhakiki uhawilishaji ardhi katika vijiji vya Nakawale na Lilahi Peramiho mkoa wa Ruvuma. Aliyevaa kofia ni mwenyekiti wa kijiji cha Nakawale Ally Paswere na kulia ni Mtendaji wa Kata ya Muhukuru halmashauri ya Songea Rajabu Issa Ajida
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akizungumza na wananchi wa kijiji cha  Nakawale halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wakati wa ziara yake ya kuhakiki uhawilishaji ardhi katika vijiji vya Nakawale na Lilahi Peramiho mkoa wa Ruvuma.
 Kaimu Kamishna wa ardhi vijijini kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Kokula Shenkumba akitoa elimu ya uhawilishaji ardhi kwa wananchi wa kijiji cha Nakawale Peramiho wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma.
 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Songea Rajabu Kiula akizungumza wakati naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula alipokwenda kuhakiki uhawilishaji ardhi katika kijiji  Nakawale Peramiho mkoani Ruvuma.
 Baadhi ya wananchi wa wa kijiji cha Nakawale Peramiho wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma  wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula (hayupo pichani)  wakati wa uhakiki wa uhawilishaji ardhi ya kijiji hicho.
 Wajumbe wa halmashauri ya Kijiji cha Lilahi Peramiho Wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma wakitambulishwa kwa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula wakati ziara ya uhakiki wa uhawilishaji ardhi ya kijiji.
 Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Kusini Gasper Luanda akizungumza wakati wa uhakiki uhawilishaji ardhi kijiji cha Lilahi Peramiho Wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akifurahia jambo na mbunge wa jimbo la Madaba mkoa wa Ruvuma Joseph Muhagama mara baada ya mkutano na wananchi wa kijiji cha Lilahi Peramiho wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad