HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 6, 2018

IGP SIRRO AFUNGA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MAAFISA WA POLISI

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akipokea salamu ya heshima ya kijeshi wakati alipowasili katika Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu mkoani Morogoro, kwa ajili ya kufunga Mafunzo ya wiki nne ya Utayari ya kuwajengea uwezo wa kukabiliana na matukio ya uhalifu na wahalifu Wakuu wa Polisi Wilaya (OCDs) na Maafisa Operesheni. Picha na Jeshi la Polisi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (wa pili kushoto), akiwa ameongozana na Naibu Kamishna wa Polisi Msataafu (DCP) Vennance Tossi (katikati) Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu (DCP) Mpinga Gyumi na baadhi ya Maafisa na askari wa Jeshi hilo wakati alipowasili katika Chuo hicho kwa ajili ya kufunga Mafunzo ya wiki nne ya Utayari ya kuwajengea uwezo wa kukabiliana na matukio ya uhalifu na wahalifu Wakuu wa Polisi Wilaya (OCDs) na Maafisa Operesheni. Picha na Jeshi la Polisi.
 Mmoja kati ya askari Polisi 203 wanaoshiriki mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo Wakuu wa Polisi Wilaya (OCDs) na Maafisa Operesheni katika Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu mkoani Morogoro akiwa katika onesho la namna ya kukabiliana na uhalifu, mafunzo hayo ya wiki nne yalifungwa jana na  Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro. Picha na Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad