HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 20, 2018

BENKI YA CRDB YAIONGEZEA MTAJI WA SH. 3.2 BILIONI BENKI YA WANANCHI TANDAHIMBA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia), akifafanua jambo mbele ya waandhishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kusaini Mkataba wa kuiwezesha Benki ya Wananchi Tandahimba (TACOBA) kimtaji iliyofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Benki ya CRDB imeipatia Benki ya Wananchi Tandahimba kiashi ya Sh. 3.2 Bilioni kuongeza mtaji wake. wengine pichani toka kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Wananchi Tandahimba (TACOBA), Rajabu Mmunda, Meneja Mkuu wa Benki ya Wananchi Tandahimba, Mugwagi Steven.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Wananchi Tandahimba (TACOBA), Rajabu Mmunda akizungumza jambo katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akibadilishana Mkataba na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Wananchi Tandahimba (TACOBA), Rajabu Mmunda  wa kuiwezesha Benki ya Wananchi Tandahimba (TACOBA) kimtaji katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad