HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 8, 2018

Benki ya CRDB na Jeshi la Polisi nchini kudumisha mahusiano ya kibiashara

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia) akizungumza wakati uongozi wa Benki ya CRDB ulipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam jana kwa ajili ya kudumisha mahusiano ya kibiashara kati ya CRDB na Jeshi hilo. Huku akisikilizwa kwa makini na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro pamoja na Kamishna wa Ushirikishwaji wa Jamii kwa Jeshi la Polisi, CP Mussa Ali Mussa. Kulia ni Naibu Mkurugenzi Benki ya CRDB Bi. Esther Kitoka.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akieleza jambo kwa baadhi ya Maafisa wa juu wa Jeshi la Polini pamoja na Wafanyakazi wa Benki ya CRDB (hawapo pichani) katika Mkutano maalum wa kudumisha mahusiano ya kibiashara kati ya CRDB na Jeshi hilo, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei na Kushoto ni Kamishna wa Ushirikishwaji wa Jamii kwa Jeshi la Polisi, CP Mussa Ali Mussa. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, akionyesha Kadi ya TemboCard Visa Infinite, aliyokabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), wakati uongozi wa Benki ya CRDB ulipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam jana kwa ajili ya kudumisha mahusiano ya kibiashara. Kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Viva Tower, Naomi Mwamfupe.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad