Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari -
MAELEZO, Rodney Thadeus akifafanua jambo mbele ya watumishi wa Idara hiyo
walipokutana na ujumbe kutoka Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwa ajili ya
kujengewa uelewa kuhusu huduma za Shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka
kulia ni Afisa Mauzo wa TTCL, Bi. Rahel Mremi na Esther Killango. TTCL ni
shirika la Serikali linalotoa huduma za mawasiliano likiwa na kauli mbiu
"Rudi Nyumbani Kumenoga."
Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL),
Bi. Rahel Mremi akionyesha Line za TTCL mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari
-MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati
ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus na Afisa
Mauzo wa TTCL, Esther Killango(kushoto).
Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL),
Bi. Esther Killango akifafanua jambo mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari
-MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka
kulia ni Msaidizi wa Mauzo wa TTCL, Bi. Damiana Shemweta, Afisa Mauzo wa TTCL,
Bi. Rahel Mremi na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney
Thadeus(wapili kutoka kushoto).
Baadhi ya watumishi wa Idara ya Habari - MAELEZO,
kituo cha Dar es Salaam wakifuatilia maelezo kuhusu huduma na bidhaa
zinazotolewa na Shirika la Simu Tanzania (TTCL) walipotembelewa na maafisa
mauzo kutoka shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.
Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL),
Bi. Rahel Mremi akionyesha moja ya aina ya simu zinazotumika kwa ajili ya
huduma ya sauti mbele ya watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea
ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi
wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus(katikati) na Afisa Mauzo wa TTCL,
Esther Killango.
Msaidizi wa mauzo toka Shirika la Simu Tanzania
(TTCL), Bi. Damiana Shemweta akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya huduma na
bidhaa za shirika hilo kwa watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO leo Jijini Dar
es Salaam. (Picha na: Frank Shija - MAELEZO)
No comments:
Post a Comment