HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 11, 2018

Watumishi MAELEZO Wakunwa na Huduma TTCL

 Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus akifafanua jambo mbele ya watumishi wa Idara hiyo walipokutana na ujumbe kutoka Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwa ajili ya kujengewa uelewa kuhusu huduma za Shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Afisa Mauzo wa TTCL, Bi. Rahel Mremi na Esther Killango. TTCL ni shirika la Serikali linalotoa huduma za mawasiliano likiwa na kauli mbiu "Rudi Nyumbani Kumenoga."
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Rahel Mremi akionyesha Line za TTCL mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus na Afisa Mauzo wa TTCL, Esther Killango(kushoto).
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Esther Killango akifafanua jambo mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Msaidizi wa Mauzo wa TTCL, Bi. Damiana Shemweta, Afisa Mauzo wa TTCL, Bi. Rahel Mremi na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus(wapili kutoka kushoto). 
 Baadhi ya watumishi wa Idara ya Habari - MAELEZO, kituo cha Dar es Salaam wakifuatilia maelezo kuhusu huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika la Simu Tanzania (TTCL) walipotembelewa na maafisa mauzo kutoka shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Rahel Mremi akionyesha moja ya aina ya simu zinazotumika kwa ajili ya huduma ya sauti mbele ya watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus(katikati) na Afisa Mauzo wa TTCL, Esther Killango.
Msaidizi wa mauzo toka Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Damiana Shemweta akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya huduma na bidhaa za shirika hilo kwa watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na: Frank Shija - MAELEZO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad