HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 24, 2018

SIMANZI ,VILIO VYATAWALA WAKATI WA KUAGA MIILI YA WATUMISHI WATATU WA KITUO CHA UWEKEZAJI TANZANIA


*Waziri Mwijage asema Taifa limepata pigo kubwa kwa kupoteza watumishi waadilifu.
*Mkurugenzi Mtendaji TIC aelezea utendaji wao, azungumzia namna alivyowaamini.

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
Ni vilio na simanzi ndivyo vilivyokuwa vimetawala katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam wakati wa kuaga miili ya watumishi wa tatu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) waliofariki dunia kwa ajali ya gari wakitokea Dar es Salaam kwenda Dodoma kikazi.

Miili hiyo ilifikishwa kwenye viwanja hivyo saa nne asubuhi leo ambapo mamia ya waombolezaji walioongozwa na Waziri Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwigaje.Wengine ni  Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali Serikali.

Watumishi hao wa TIC ambao miili yao imeagwa leo viwanjani hapo ni aliyekuwa Mkurugenzi Idara ya Utafiti,Mipango na Mifumo ya Mawasiliano Said Amiri Moshi, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za kitaasisi Zacharia Kingu Meneja Utafiti Martin Masalu

Akizungumza mbele ya mamia ya waombolezaji,Waziri Mwijage amesema vifo vya watumishi hao ni pigo kubwa kwa TIC, Taifa na familia kwa ujumla na enzi za uhai wao walikuwa vijana walioonesha umahiri mkubwa wa kiutumishi.

Amesema kwake yeye watumishi hao walikuwa ni marafiki zake na anachoweza kukilezea  anatambua mchango wa kila mmoja wao kutokana na utendaji kazi wa kizalendo  waliouonesha kwenye kituo hicho.

Amesema waliaminiwa na kupewa majukumu makubwa hasa kwa kuzingatia walikuwa na uelewa mkubwa kuhusu masuala ya uwekezaji.

"Nikiri vijana hao wameacha pigo kubwa kwetu hasa kipindi hiki ambacho tupo kwenye mchakato wa ujenzi wa viwanda nchini.Hata hivyo vijana wengine waliobakia TIC waendelea kutekeleza majukumu yao kwa maslahi ya nchi yetu.

 "Watumishi hawa ambao leo tunawaaga walifariki wakiwa njiani kelekea Dodoma kwa ajili ya kutekeleza majukumu muhimu.Tunafahamu kuna baadhi ya changamoto  ambazo zipo kwenye uwekezaji hivyo walikuwa wanakwenda kwenye kikao kuwaambia watendaji wa Serikali mambo muhimu ya kuvutia uwekezaji nchini,"amesema.

Amesema wakati anapata taarifa hizo za msiba alipatwa na mshtuko na hakujua afanye nini lakini kwa kuwa imetokea, kilichobaki watendaji wa TIC kuendelea na ujenzi wa nchi yao huku akifafanua haina tofauti na vitani askari mmoja akitangulia mbele ya haki basi waliobakia wanachukua silaha wanatakiwa kusonga mbele kwani kinyume na hapo taifa litapata hasara.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Mwambe amesema vifo vya watumishi hao ni pigo kubwa kwao hasa kwa kuzingatia ni walikuwa watumishi ambao walitekeleza majukumu yao bila kuchoka na kutanguliza uzalendo kwa nchi yao.

Amesema watumishi hao hata pale ambapo alikuwa akipata safari za kikazi hakusita kuwaachia ofisini kuendelea na majukumu ya kituo hicho na kufafanua TIC imeamua kugharamia shughuli zote za mazishi ya watumishi hao huku akielezea namna ambavyo wameumizwa na vifo hivyo.

Mwambe ameelezea namna ambavyo watumishi hao kila mmoja kwa nafasi yake enzi za uhai wao walivyokuwa muhimili na kiunganishi muhimu kwa wawekezaji wa ndani na  nje , hivyo wameacha pigo kubwa.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza jambo kwa ndugu na jamaa wa marehemu wakati kuagwa kwa miili ya watumishi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kwenye ukumbi wa Kareemjee jijini  Dar es Salaam.
MkurugenziMtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Geoffrey Mwambe akizungumza na mbele ya waombolezaji walioshiriki kuaga miili ya watumishi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kwenye ukumbi wa Kareemjee jijini  Dar es Salaam.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Hamphrey Polepole akitoa neo la pole kwa ndugu na jamaa wa marehemu wakati wa kuagwa kwa miili ya wafanyakazi wa TIC.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akitoa heshima ya mwisho kwenye miili ya watumishi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC).
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola akiaga  miili ya watumishi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC)
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Hamphrey Polepole akitoa heshima za mwisho kwenye miili ya watumishi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC)
Mkurugenzi Mtendaji wa Zamani  wa TIC na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari(katikati) akiaga miili ya wafanyakazi wa TIC.
 Wafanyakazi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) wakitoa salamu za pole kwa ndugu na jamaa wa marehemu waliofariki dunia kwa ajali ya gari wakitokea Dar es Salaam kwenda Dodoma kikazi.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad