HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 19, 2018

MKUTANO MKUU WA 23 WA BENKI YA CRDB WAFANYIKA LEO JIJINI ARUSHA, WANAHISA WAMTAKA DKT. KIMEI KUENDELEA KUIONGOZA BENKI YAO

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza wakati akitoa taarifa ya Benki kwa Wanahisa wa Benki hiyo, katika Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Simba uliopo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018. Katika Mkutano huo, Sehemu kubwa ya wajumbe wamemuomba Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo,  Dkt. Charles Kimei kuendelea kuitumikia nafasi yake hiyo, ya kuingoza benki hiyo kwa miaka mingine mitano. 

Hatua hiyo ilifikia pindi, Dkt. Kimei alipowajulisha wanahisa hao wakati alipokuwa akitoa hotuba ya mwenendo wa benki, kuwa kwenye mkutano mkuu ujao, atawaaga rasmi baada ya kumaliza muda wake wa kuitumia Benki hiyo.

Kwenye michango yao, baadhi ya wanahisa hao walisema hiki ni kipindi kigumu kiuchumi hivyo CRDB inahitaji mtu mwenye uzoefu wa kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo. Mmoja wa wanahisa hao, Emburis Sirikwa wa Arusha alisema endapo mkurugenzi huyo ataondoka na kuiacha benki hiyo, ndani ya miaka miwili ya kutokuwanaye lazima ufanisi utapungua.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Laay akizunguza katika Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Simba uliopo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018. 
Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, Abeid Mwasajone akizungumza jambo kwa wajumbe wa Mkutano huo, unaofanyika leo Mei 19, 2018 kwenye Ukumbi wa Simba uliopo ndani ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC, Jijini Arusha.
 Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, wakiwa kwenye Mkutano huo, unaofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Simba wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018.
Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, unaofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Simba wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018.

Sehemu ya Wanahisa wa Benki ya CRDB wakichangia mada mbalimbali zinazoendelea kutolewa katika Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, unaofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Simba wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018.
Mtangazaji wa zamani wa Radio Tanzania na Mwanahisa wa Benki ya CRDB, Mzee Salim Mbonde akichangia mada katika Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB, unaofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Simba wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC), jijini Arusha leo Mei 19, 2018.














































































No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad