HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 5, 2018

KAMATI YA BUNGE YA KUDUMU YA UTAWALA NA SERIKALI YAFANYA ZIARA TAGLA JIJINI DAR

 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, wakiwa katika mkutano ulioendeshwa kwa kwa njia ya video kwa kuunaga na wadau waliokuwepo Dodoma, Arusha na Nairobi nchini Kenya, wakiwa katika ukumbi wa Mikutano wa Wakala wa Mafunzo kwa njia ya Mtandao (TaGLA), uliopo kwenye Jengo la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), jijini Dar es salaam leo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Mafunzo kwa njia ya Mtandao (TaGLA), Charles Senkondo akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, waliofanya ziara kwenye ofisi zao, zilizopo kwenye Jengo la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), jijini Dar es salaam leo.
 Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, wakifatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye Mkutano huo.
 Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Venance Mwamoto (picha ya kushoto) akiuliza swali katika Mkutano huo kupitia teknolojia video.  


 Meneja wa Wakala wa Mafunzo kwa njia ya Mtandao (TaGLA), Emmanuel Tessua akieleza jambo kwa Ujumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, wakati walipotembelea Chumba cha kuunganishia mitambo ya TaGLA.  
 Afisa Rasilimali watu wa Wakala wa Mafunzo kwa njia ya Mtandao (TaGLA), Fredrick Massawe (kushoto) akiwaeleza jambo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa.



1 comment:

  1. Tunashukuru Wajumbe wa kamati ya kudumu ya utawala na Serikali za mitaa kufika na kuona kazi za Tanzania Global Learning agency (TaGLA).

    ReplyDelete

Post Bottom Ad