Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kuzungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada, Balozi Alphayo Kidata, ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi Kidata ambaye aliapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada tarehe 10, Mei 2018 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi Kidata alifika leo kuona Makamu wa Rais na kumuaga rasmi tayari kwa kwenda kulitumikia Taifa kwenye kituo chake kipya cha kazi nchini Canada.
Makamu wa Rais, Mhe. Samia amempongeza na kumtakia kazi njema ambapo alimtaka kwenda kufanya yale nchi imeelekeza haswa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya Uchumi wa Viwanda.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na
Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Mhe. Alphayo Kidata aliyefika
ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la
kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi. (Picha na Ofisi
ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Mhe.
Alphayo Kidata aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es
Salaam kwa lengo la kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha
kazi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Canada Mhe.
Alphayo Kidata mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es
Salaam kwa lengo la kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha
kazi.
(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
No comments:
Post a Comment