HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 10, 2018

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA SPIKA WA EALA, BALOZI MDOGO WA MAREKANI NCHINI TANZANIA.

 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Dkt. Inmi Patterson (kulia) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Dkt. Inmi Patterson (kulia) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akikabidhiwa zawadi ya kitabu kutoka kwa Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Martin Ngoga (kushoto) pale ugeni kutoka Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. Ikiwa ni maandalizi kabla ya kuanza kamati za Bunge hilo leo, ikifuatiwa na vikao vitakavyoanza tarehe 17 Aprili, 2018 mpaka tarehe 26 Aprili, 2018 Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kulia) akizungumza na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Martin Ngoga (kushoto) pale ugeni kutoka Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. Ikiwa ni maandalizi ya kamati za Bunge hilo linaloanza leo, ikifuatiwa na vikao vitakavyoanza tarehe 17 Aprili, 2018 mpaka Tarehe 26 Aprili, 2018 vitakavyofanyika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na bendera ya Bunge hilo walioongozwa na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Martin Ngoga (watatu kushoto) pale ugeni kutoka Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. Ikiwa ni maandalizi ya kamati za Bunge hilo linaloanza leo tarehe 10 Machi, 2018, ikifuatiwa na vikao vitakavyoanza tarehe 17 Aprili, 2018 mpaka Tarehe 26 Aprili, 2018 vitakavyofanyika Mjini Dodoma.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad