HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 13, 2018

MKURUGENZI HUDUMA ZA UFUNDI SEKTA YA UJENZI AFUNGUA BARAZA LA WAFANYAKAZI TEMESA

 Mtendaji mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA, Dkt. Mussa Mgwatu akisoma taarifa kwa mgeni rasmi, wajumbe na watendaji hawapo pichani wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa wakala huo Hans Lyimo, Mkurugenzi wa Huduma za  ufundi sekta ya ujenzi Mhandisi William Nshama na Afisa Rasilimali watu kutoka wakala huo Evarista Asenga.
 Mkurugenzi wa Huduma za ufundi sekta ya ujenzi, Mhandisi William Nshama akizungumza wakati akifungua kikao cha baraza la wafanyakazi TEMESA na wajumbe na baadhi ya watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA hawapo pichani katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mtendaji mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa wakala huo Hans Lyimo.
 Naibu katibu mkuu wa TUGHE Taifa Mhandisi Amani Msuya kulia akiimba wimbo wa wafanyakazi mshikamano daima pamoja na Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Ferdinand Mishamo wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot jijini Dar es Salaam. 
 Naibu katibu mkuu wa TUGHE Taifa Mhandisi Amani Msuya akifafanua jambo kwa wajumbe na baadhi ya wafanyakazi wa wakala hawapo pichani wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya wajumbe, mameneja na watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA waliohudhuria kikao cha Baraza la wafanyakazi TEMESA wakisikiliza kwa umakini mada zilizokuwa zikitolewa katika kikao hicho cha baraza kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Mt Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za ufundi sekta ya ujenzi Mhandisi William Nshama katikati akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA mara baada ya kuzindua na kufungua mkutano wa baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano Mt Depot Keko jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO TEMESA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad