Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
ALIYEKUWA Rais wa Brazil Luiz Inancio Lula da Silva maarufu kama Lula ametakiwa kuanza kutumikia kifungo chake cha miaka 12 gerezani kwa tuhuma za rushwa ya Euro laki saba na tisini wakati wa utawala wake.
Licha ya Lula kukanusha madai hayo nusu ya majaji waliunga mkono kifungo cha da Silva licha ya wananchi wengi kutegemea mkongwe huyu wa siasa kuekana katika mbio za uchaguzi mkuu utakaofanyika mapema Octoba.
Lula anaungwa mkono na wafuasi wake katika miji ya Sao na Bernardo ambao waliandamana kupinga adhabu hii na kutaka aachiwe huru.
Luiz Inancio da silva (72) alizaliwa October 27, 1945 akiwa Rais wa 35 kuiongoza Brazil kuanzia Januari 1 2003 hadi Januari 1 2011 na ikumbukwe kuwa Lula alikuwa rafiki wa karibu wa aliyekuwa kiongozi wa Cuba Fidel Castro.
No comments:
Post a Comment