HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 13, 2018

VITUO VYA AFYA CHALINZE HAVINA VYUMBA VYA KUHIFADHIA MAITI

Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze
MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ,ameweka wazi kuwa vituo vya afya katika jimbo hilo vinakabiliwana na ukosefu wa vyumba vya kuhifadhia maiti .

Amesema changamoto hiyo ni kubwa ambapo husababisha wananchi kupeleka maiti za ndugu zao kwenye Hospitali teule ya rufaa ya Tumbi na wilaya ya Bagamoyo ambako kuna mbali mrefu.

Aliyasema hayo mjini Chalinze,wakati akizungumza na baadhi ya wananchi,na kusema  shida kubwa inatokea hasa pale mgonjwa anapokuwa amefariki.

Ridhiwani alisema jimbo zima la Chalinze hakuna chumba cha kuhifadhia maiti kwenye vituo vyote vya afya hali ambayo imekuwa mtihani mkubwa kwa wananchi wa jimbo hilo .

"Hali ni mbaya kwa wenzetu wa kata ya Kibindu ambao wanapeleka maiti Hospitali ya Bwagala wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro ,”

"Wananchi wanaingia gharama kwenda kuhifadhi maiti sehemu nyingine ambako ni mbali na maeneo yao"

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za afya kwenye vituo vya afya pamoja na zahanati lakini changamoto yetu kubwa ni ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti ambapo tunajitahidi kufanya njia ili kuhakikisha tunajenga chumba hicho,” alisema Ridhiwani.

Hata hivyo, Ridhiwani alisema kata ya Lugoba ambapo kuna kituo cha afya serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kujenga majengo yakiwemo wodi ya mama na mtoto, maabara, chumba cha kufanyia upasuaji mdogo kwa ajili ya akinamama na chumba cha kuhifadhia maiti.


Akielezea suala hilo ,mkuu wa mkoa wa Pwani ,Mhandisi  Evarist Ndikilo alisema serikali inaendelea na uboreshaji wa huduma za afya kwenye zahanati zake 292 na vituo vya afya 26 ambapo vituo 119 vimekarabatiwa ili kutoa huduma bora.

Alisema mbali ya hilo pia inahakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa mkubwa.

Ndikilo alieleza kwa sasa ni kunahakikishwa kunakuwa na ongezeko kutoka asilimia 73.3 hadi kufikia asilimia 85 hali ambayo amesema inawezekana kutokana na mikakati iliyowekwa ya upatikanaji wa dawa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad