HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 10, 2018

TATU MZUKA YAKABIDHTI KALENDA 500 KWA JESHI LA POLISI,IGP SIRRO ATOA NENO

Kampuni ya Bahati Nasibu Tatu Mzuka imekabidhi kalenda 500 kwa Jeshi la Polisi nchini,kama mwanzo wa uhusiano mwema utakaozaa matunda kati ya Tatu Mzuka na Jeshi la Polisi. 

Akizungumza na waandishi habari wakati makabidhiano ya kalenda kwa Jeshi la Polisi mapema jana , Msemaji wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga amesema wameamua kutengeneza kalenda 500 za Jeshi la Polisi kama sehemu ya kujenga uhusiano bora, lakini pia kuendeleza kauli mbiu ya Tatu Mzuka ya ukishinda Tanzania inashinda pia. 

Maganga amesema wao ni raia wema wa Tanzania hivyo ni nafasi ya pekee kuwa mbele kutokana na kazi ambayo inafanya jeshi la Polisi katika kulinda watu na mali zao chini ya Mkuu wa Jeshi la Polisi(IGP), Simon Sirro,na kwamba Kauli mbiu ya Tatu Mzuka “Ukishinda Tanzania inashinda”, 

“Mchezo wa bahati nasibu wameweza kushirikiana na Mkuu wa wilaya ya Temeke katika kusaidia ujenzi wa kituo cha polisi kuwasaidia wananchi wa Mbande baada ya mapolisi kuuliwa kwa kutokuwa na kituo maeneo ya karibu. " Tumefanya kitu hiki kwa niaba ya washindi wa mchezo wetu wa bahati nasibu,ambao mpaka sasa wamefikia idadi ya milioni 6 ambao wote wamehakikishiwa usalama wao na jeshi la polisi.

Mkuu wa jeshi la Polisi ( IGP ) Simon Sirro ameeleza kuukubali mchezo wa kubahatisha nchini wa Tatu Mzuka unaoshika kasi kwa kubadilisha maisha ya Watanzania wengi. 

IGP Sirro amesema hayo wakati akipokea kalenda za jeshi hilo zilizokabidhiwa na viongozi wa Tatu Mzuka kwenye makao makuu ya Jeshi la Polisi, Posta jijini Dar es Salaam juzi."Mmefanya jambo jema lakini pia mmeonyesha mfano kwa wengine, binafsi nimeguswa na mwamko wenu, hongereni sana na endeleeni kuchapa kazi," alisema IGP Sirro. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro akikabidhiwa moja ya Kalenda kati ya 500 zilizotolewa na Kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ya Tatu Mzuka,kutoka kwa Mratibu wa Mawasiliano kampuni hiyo Sebastian Maganga (pichani kati).kulia ni Mmoja wa Wakilishi Simon Simalenga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akikabidhiwa moja ya faluna ya Tatu Mzuka kutoka kwa  Mratibu wa Mawasiliano  Tatu Mzuka, Sebastian  Maganga (pichani kati).kulia ni Mmoja wa Wakilishi Simon Simalenga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad